Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro
SERENGETI, MARA
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro amewataka wananchi kuacha kujihusisha na vitendo vya ukiukwaji wa maadili jambo linalopelekea vitendovya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto.
IGP Sirro amesema hayo leo wakati akizindua Ofisi za dawati la jinsia na watotoMugumu wilayani Serengeti mkoani Mara ambapo wananchi wametakiwakwenda kuripoti matukio ya ukatili hili hatua ziweze kuchukuliwa.
Aidha, IGP Sirro ameendelea kuwaonya wananchi kuacha mara moja vitendo
vya kihalifu hususani wizi wa mifugo.
Naye Mkurugenzi wa Shirika la Utu wa Mtoto (CDF) bwana Koshuma Mtengete amesema kuwa, ni vyema jamii ikaendelea kuelimika kwa kutoa taarifa za unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto ikiwa ni sambamba na kutokufumbia macho vitendo hivyo.
Kwa upande Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ya
Serengeti ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo Nurdin Babu amesema kuwa,
wilaya yake imeendelea kutoa elimu kwa kuwaelimisha wananchi hususan
kwenye masuala ya kiusalama ikiwemo kuachana na mila kandamizi na
zilizokwisha kupitwa na wakati.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...