Kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Swedy Mkwabi, Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Simba Sports Club Limited imemteua, Mwina Kaduguda kuwa Kaimu Mwenyekiti wa Klabu hiyo.

Taarifa kwa Umma iliyotolewa mapema leo na Klabu hiyo, imeeleza uteuzi huo umeanza leo Novemba 19, 2019. Tarehe ya Uchaguzi kujaza nafasi ya Mwenyekiti wa Klabu hiyo utatangazwa na Bodi ya Wakurugenzi hapo baadae.

Hata hivyo, Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Simba Sports Club imemteua, Salim Abdallah Muhene kuwa Makmu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni hiyo, kwa uteuzi huo kuanza leo.

Taarifa hiyo imeeleza teuzi hizo zimefanywa kwa mujibu wa Mamlaka ya Bodi chini ya Ibara ya 50 ya Katiba ya Klabu ya Simba yam waka 2018.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...