Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na Mkurugenzi
wa Shirika la Kimataifa la Wakimbizi (UNHCR), Kanda ya Mashariki, Pembe ya
Afrika na Maziwa Makuu, Clementine
Nkweta-Salami (kulia). Mazungumzo hayo yalifanyika katika ofisi ya Naibu Waziri,
jijini Dodoma, leo. Wapili kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika hilo Nchini, Chansa
Kapaya.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akimsikiliza
Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Wakimbizi (UNHCR), Kanda ya Mashariki,
Pembe ya Afrika na Maziwa Makuu,
Clementine Nkweta-Salami, alipokuwa anamfafanulia jambo katika
mazungumzo yao yaliyofanyika jijini Dodoma, leo. Kushoto ni Mwakilishi Mkazi wa
Shirika hilo Nchini, Chansa Kapaya.
Naibu Waziri wa Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto), akiagana na Mkurugenzi wa
Shirika la Kimataifa la Wakimbizi (UNHCR), Kanda ya Mashariki, Pembe ya Afrika
na Maziwa Makuu, Clementine
Nkweta-Salami, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika ofisi za Wizara
hiyo, jijini Dodoma, leo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi.
Na Mwandishi Wetu, MOHA, Dodoma.
NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amefanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Wakimbizi (UNHCR), Kanda ya Mashariki, Pembe ya Afrika na Maziwa Makuu, Clementine Nkweta-Salami, na kumuhakikishia ushirikiano zaidi kati ya Wizara yake na Shirika hilo.
Mazungumzo hayo ya zaidi ya saa moja yalifanyika ofisini kwa Mhandisi Masauni, jijini Dodoma, leo ambayo yalijadili masuala mbalimbali ikiwemo uimarishaji wa ushirikiano hasa katika kuhakikisha wakimbizi wanalindwa na kuhudumiwa ipasavyo.
Naibu Waziri Masauni alimuhakikishia Mkurugenzi huyo Tanzania itaendelea kulinda haki za wakimbizi kama ilivyokuwa kwa miaka mingi, na pia inasimamia zoezi la kuwarejesha kwa hiari nchini kwao Wakimbizi kutoka Burundi.
“Nikuhakikishie tu, Serikali ya Tanzania inawajali wakimbizi, ndio maana kwa miaka mingi inaendelea kuwahifadhi, hivyo katika kipindi hiki cha kuwarejesha nchini kwao tunahakikisha wanarudishwa wakimbizi wote kwa hiari,” alisema Masauni.
Aidha, Masauni alisema mazungumzo zaidi kuhusu wakimbizi waliopo nchini yatajadiliwa zaidi na kukubaliana katika mkutano wa pande tatu unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni.
Naibu Waziri alimshukuru Mkurugenzi huyo ambaye aliambatana na Mwakilishi Mkazi wa Shirika hilo hapa nchini, Chansa Kapaya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...