Mbunge wa Mafinga Cosato Chumi amewapongeza Wanachama wa Yanga Tawi la Mafinga, maarufu kama Vanyalutogo kwa juhudi za kutatua changamoto katika jamii.
Chumi amesema kitendo walichokifanya ni uwanamichezo uliotukuka ambapo kwanza walianza na tanki la.maji na sasa wameleta pampu za kuvutia maji.
“Hongereni sana Yanga Mafinga, huu ni uwanamichezo uliotukuka, kwanza mlianza na Tanki la maji, lakini tena mkajiongeza mumekabidhi na pump. Huu ni uzalendo wa kimichezo.”amesema Chumi.
Tawi hilo la Mafinga limetoa msaada wa Tanki la Maji na Mashine ya kuvuta maji (Water Pump) kwa Shule ya Sekondari ya Iyongole.
Wanachama hao wakiongozwa na Mwenyekiti wao tawi Gift Mwachang'a wamwtoa vifaa hivyo kwa wanafunzi ili kiutatua changamoto ya maji kwenye shule hiyo.
“Vifaa hivi vyote vimetolewa na Wanayanga wenyewe, hii ni Timu ya Wananchi na tunawafikia Wananchi kwa namna mbalimbali,” Mwachang’a.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...