Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa amewataka wananchi kujiwekea utaratibu wa kujikatia bima ya afya na kuacha kutumia pesa nyingi katika mambo ya anasa na kusahau kuhusu afya zao
Mhe. Byakanwa amesema hayo leo 19.12.2019 wakati wa Uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na vifurushi vya bima ya afya Mkoani Mtwara
Mhe. Byakanwa amesema kuwa umekuwa ni utaratibu kwa watanzania wengi kupeleka fedha nyingi katika vyama vya kufa na kuzikana badala ya kuwekeza fedha hizo katika afya zao.
“Ni lazima watanzania tubadilike, afya ndio kila kitu, watanzania tumekuwa wachangiaji wakubwa kwenye mambo ya anasa na kusahau kuwa afya ndio msingi wa mambo hayo yote, NHIF wamepunguza gharama kutoka Milioni Moja na Laki tano za hapo awali na sasa unalipa laki moja na tisini ta mbili tu kwa mwaka mzima kwa mtu mmoja, tujiunge tuwe na uhakika wa matibabu”-Alisema Byakanwa.
Mhe. Byakanwa amesema hayo leo 19.12.2019 wakati wa Uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na vifurushi vya bima ya afya Mkoani Mtwara
Mhe. Byakanwa amesema kuwa umekuwa ni utaratibu kwa watanzania wengi kupeleka fedha nyingi katika vyama vya kufa na kuzikana badala ya kuwekeza fedha hizo katika afya zao.
“Ni lazima watanzania tubadilike, afya ndio kila kitu, watanzania tumekuwa wachangiaji wakubwa kwenye mambo ya anasa na kusahau kuwa afya ndio msingi wa mambo hayo yote, NHIF wamepunguza gharama kutoka Milioni Moja na Laki tano za hapo awali na sasa unalipa laki moja na tisini ta mbili tu kwa mwaka mzima kwa mtu mmoja, tujiunge tuwe na uhakika wa matibabu”-Alisema Byakanwa.
Aidha, Byakanwa alisema kuwa Mpango huu wa Vifurushi vya Bima ya Afya ni msingi wa kujenga taifa lenye uwezo wa kuzalisha mali, taifa lilio tayari kwenda katika uchumi wa kati, taifa lililo tayari kujenga uchumi wa viwanda na taifa lenye watu wenye afya njema
Akioongea wakati wa uzinduzi huo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mhe. Anne Makinda alisisitiza kuwa taifa lolote lenye kuhitaji maendeleo lazima liwe na wananchi wenye afya hivyo watanzania hawana budi kuweka utaratibu wa kukata Bima ya Afya ili kuwa na uhakika wa matibabu.
Akioongea wakati wa uzinduzi huo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mhe. Anne Makinda alisisitiza kuwa taifa lolote lenye kuhitaji maendeleo lazima liwe na wananchi wenye afya hivyo watanzania hawana budi kuweka utaratibu wa kukata Bima ya Afya ili kuwa na uhakika wa matibabu.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Evod Mmanda aliwapongeza NHIF kwa kuja na mpango huu wa Vifurushi vya Bima ya Afya vitakavyowezesha idadi kubwa ya watanzania kuwa na Bima ya Afya.
Wakati huohuo Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bw. Bernard Konga alisema kuwa waliamua kubuni mpango wa vifurushi ili kuhakikisha kuwa kila mtanzania anapata huduma ya Bima ya Afya na anakuwa na uhakika wa matibabu.
Mbunge wa Jimbo la Nanyamba Mhe. Abdallah Chikota aliishukuru NHIF kuja na mpango huu kwani bunge limekuwa liibana serikali kwa muda mrefu kuhakikisha wanakuja na mpango ambao utawajumuisha watanzania wengi zaidi.
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umezindua vifurushi vipya vya Bima ya Afya vilivyopewa majina ya NAJALI AFYA, TIMIZA AFYA na WEKEZA AFYA vyenye lengo la kujumuisha watanzania wengi zaidi hasa walio katika ajira zisizo rasmi.
Wakati huohuo Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bw. Bernard Konga alisema kuwa waliamua kubuni mpango wa vifurushi ili kuhakikisha kuwa kila mtanzania anapata huduma ya Bima ya Afya na anakuwa na uhakika wa matibabu.
Mbunge wa Jimbo la Nanyamba Mhe. Abdallah Chikota aliishukuru NHIF kuja na mpango huu kwani bunge limekuwa liibana serikali kwa muda mrefu kuhakikisha wanakuja na mpango ambao utawajumuisha watanzania wengi zaidi.
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umezindua vifurushi vipya vya Bima ya Afya vilivyopewa majina ya NAJALI AFYA, TIMIZA AFYA na WEKEZA AFYA vyenye lengo la kujumuisha watanzania wengi zaidi hasa walio katika ajira zisizo rasmi.
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa akiongea wakati wa Uzinduzi wa
kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na vifurushi vya bima ya afya
ambapo aliwataka wananchi kujiwekea utaratibu wa kukata bima na kuifanya
afya kuwa kipaumbele hasa baada ya NHIF kupunguza gharama na kujiunga
kwa mtu mmoja mmoja, leo 19.12.2019 Mkoani Mtwara.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mhe.
Anne Makinda akiongea wa Uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi
kujiunga na vifurushi vya bima ya afya ambapo alisisitiza kuwa taifa
lolote lenye kuhitaji maendeleo lazima liwe na wananchi wenye afya hivyo
watanzania hawana budi kuweka utaratibu wa kukata Bima ya Afya ili kuwa
na uhakika wa matibabu.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bw. Bernard Konga
kiongea wakati wa Uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga
na vifurushi vya bima ya afya ambapo alisema kuwa waliamua kubuni mpango
wa vifurushi ili kuhakikisha kuwa kila mtanzania anakuwa na huduma ya
Bima ya Afya na uhakika wa matibabu.
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Evod Mmanda Byakanwa akiongea wakati wa
Uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na vifurushi vya
bima ya afya, ambapo aliwapongeza NHIF kwa kuja na mpango huu wa
Vifurushi vya Bima ya Afya vitakavyowezesha idadi kubwa ya watanzania
kuwa na Bima ya Afya
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa akiwapa Vitambulisho vya Bima
ya Afya baadhi ya wakazi wa Mkoa huo ambao wamefanikiwa kujiunga na
mpango wa Vifurushi
Baadhi ya wananchi wakifuatilia tukio la Uzinduzi wa kampeni ya
kuhamasisha wananchi kujiunga na vifurushi vya bima ya afya leo Mkoani
Mtwara


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...