Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akizungumza na vyombo vya habari jijini Dodoma wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mpango wa Elimu kwa Umma kuhusu Sera, Sheria na Kanuni za Huduma Ndogo za Fedha, Jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.
Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akimkabidhi nakala za vitabu Kaimu
Kamishna Msaaidizi wa Idara ya Maendeleo ya Sekta ya Fedha wa Wizara ya
Fedha na Mipango Bi. Dionisia Mjema, baada ya uzinduzi wa Mpango wa
Elimu kwa Umma kuhusu Sera, Sheria na Kanuni za Huduma Ndogo za Fedha,
Jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.
Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa
Mpango wa Elimu kwa Umma kuhusu Sera, Sheria na Kanuni za Huduma Ndogo
za Fedha, kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Benki Kuu (BoT), Kanda ya Kati
Bw. Richard Wambali, Kaimu
Kamishna Msaaidizi Idara ya Maendeleo ya Sekta ya Fedha wa Wizara ya
Fedha naMipango Bi. Dionisia Mjema, , kutoka kulia ni Mkurugenzi wa
Uendeshaji wa Mfuko wa Kuendeleza Sekta ya Fedha (FSDT) Bi. Irene Mlola
na Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa TAMISEMI Bw. John Cheyo.
Mkurugenzi wa Benki Kuu (BoT), Kanda ya Kati, Bw. Richard Wambali, akizungumza
jambo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mpango wa Elimu kwa Umma kuhusu
Sera, Sheria na Kanuni za Huduma Ndogo za Fedha, Jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.
Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (katikati) na wadau wengine wakiangalia
makala kabla ya uzinduzi wa Mpango wa Elimu kwa Umma kuhusu Sera, Sheria
na Kanuni za Huduma Ndogo za Fedha, Jijini Dodoma.
Baadhi ya Wakuu wa Idara, Vitengo
na Wawakilishi wa Wakuu wa Idara na Vitengo wakisikiliza hotuba ya
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (hayupo
pichani), wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mpango wa Elimu kwa Umma kuhusu
Sera, Sheria na Kanuni za Huduma Ndogo za Fedha jijini Dodoma

Waziri wa Fedha
na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akiwa katika picha ya
pamoja na Wawakilishi wa Taasisi mbalimbali baada ya kuwakabidhi nakala
za vitabu alivyozindua kuhusu Mpango wa Elimu kwa Umma kuhusu Sera,
Sheria na Kanuni za Huduma Ndogo za Fedha jijini Dodoma.(Picha na Josephine Majura – WFM Dodoma).
………………
Na. Peter Haule na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Waziri wa Fedha
na Mipango Dkt. Philip Mpango, ameiagiza Benki Kuu ya Tanzania (BoT)
kusimamia Sekta Ndogo ya Fedha kikamilifu ili kukomesha michezo michafu
inayofanywa na baadhi ya watoa huduma ndogo za fedha nchini na
kusababisha upotevu wa mali za wananchi.
Ametoa maagizo
hayo, wakati akizindua Mpango wa Elimu kwa Umma kuhusu Sera, Sheria na
Kanuni za Huduma Ndogo za Fedha, uliowakutanisha wadau mbalimbali
zikiwemo Wizara, Idara, Taasisi na watoa huduma za fedha.
Alisema kuwa
kuna taasisi za huduma ndogo za fedha ambazo zinatoa mikopo kwa masharti
magumu ikiwa ni pamoja na viwango vikubwa vya riba na tozo ambazo
huanzia asilimia 3 mpaka asilimia 20 kwa mwezi ambayo ni sawa na
asilimia 36 mpaka 240 kwa mwaka na pia kukosekana kwa uwazi na masharti
ya mikataba ya mikopo.
‘’Naiagiza Benki
Kuu ya Tanzania ifuatilie kwa makini mwenendo wa utoaji wa huduma ndogo
za fedha kupitia mitandao (Digital Microfinance Services) na pia elimu
kwa umma ya huduma hiyo ya fedha iwe endelevu na itolewe nchi nzima”,
alieleza Dkt. Mpango.
Dkt. Mpango
alisema kuwa kwa muda mrefu takribani wananchi milioni 15.4 sawa na
asilimia 55.3 ya nguvu kazi ya Taifa walikua wanatumia huduma ndogo za
fedha bila kuwepo kwa Sheria ya kutambua na kulinda haki zao.
Aidha alisema
kutokuwepo kwa sheria inayosimamia huduma hizo za kifedha kulisababisha
kukosekana kwa uwazi wa masharti ya mikataba ya mikopo kwa kutopatikana
kwa takwimu sahihi za uendeshaji za watoa huduma hizo.
Dkt. Mpango
alisema kuwa ili kukabiliana na changamoto hizo, Serikali ilitunga
Sheria ya huduma Ndogo za Fedha ya mwaka 2018 pamoja na Kanuni zake
zilizotungwa mwaka 2019, ambazo lengo lake ni kuhakikisha watumiaji wa
huduma hizo wanalindwa kikamilifu.
‘’Sheria hii
inatambua madaraja manne ya taasisi zinazotoa huduma za fedha ambapo
Daraja la Kwanza ni zile zinazopokea amana, daraja la pili ni taasisi
zisizopokea amana, daraja la tatu linahusu vyama vya Ushirika wa Akiba
na Mikopo (SACCOS) na daraja la nne ni vikundi vya kijamii vya huduma
ndogo za fedha”, aliongeza Dkt. Mpango.
Kwa upande wake
Mkurugenzi wa BoT tawi la Kanda ya Kati, Bw. Richard Wambali, ambaye
alimwakilisha Gavana wa Benki hiyo Prof. Florens Luoga, amewataka watoa
huduma ndogo za fedha kuisoma na kuielewa sheria na kanuni zake ili
wazitekeleze kwa ufanisi.
Pia amewataka
wadau hao kutumia muda wa miezi 12 iliyotolewa na Sheria kuweka mifumo
na taratibu za biashara kuendana na matakwa ya Sheria na Kanuni ili
ifikapo Oktoba 31, 2020, muda mbao umeainishwa kisheria kuwa ni mwisho
wa kutekeleza masharti hayo wawe wamepata leseni hizo kutoka BoT au kwa
mamlaka zilizokasimishwa majukumu hayo.
Aidha amewataka
kuzingatia mazingira na fursa mbalimbali zinazotokana na uwepo wa Sheria
na Kanuni kuongeza kasi ya utoaji huduma kwa wananchi ambao
hawajafikiwa na sekta rasmi ya fedha.
Naye Mkurugenzi
wa Uendeshaji wa Mfuko wa kuendeleza Sekta ya Fedha (FSDT), Bi. Irene
Mlola, alisema kuwa Mfuko huo utaendelea kushirikiana kwa karibu na
Wizara ya Fedha na Mipango kwa kuwa anaamini nafasi ya huduma za
kifedha katika kumkomboa mwananchi kwenye hali ya uchumi na kumsaidia
kimaendeleo katika kupunguza umasikini.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...