Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

SUALA la baadhi ya mitandao ya simu nchini kufunga laini  kabla ya tarehe elekezi ya kufunga laini hizo ambayo ni Desemba 31 mwaka huu.
 
Waziri mwenye dhamana ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe amesema kuwa kufikia Desemba 31 laini zote za simu ambazo hazijasajiliwa kwa alama za vidole na namba za kitambulisho cha uraia zinazotolewa na (NIDA) zitakatwa na kile kinachoelezwa kuwa baadhi ya mitandao imeanza kufunga laini hizo ni kukumbushwa kuwa watazikata laini zote zisizo na usajili.

Akijibu hoja ya kwanini baadhi ya makampuni ya simu yamefunga laini za simu kabla ya wakati Mhandisi Kamwelwe amesema;

"Zoezi la usajili litakamilika tarehe 31 Desemba mwaka huu, na tutakata laini zote zisizosajiliwa kwa kutumia namba za NIDA na alama  za vidole" amesema.

Aidha amesema kuwa watanzania wengi wamekuwa wakiibiwa kutokana na umiliki holela wa laini za simu ambapo mtu mmoja anaweza kumiliki laini za simu zaidi ya mia moja.

"Kenge hasikii hadi damu itoke puani, mlikuwa mnashtuliwa tutakata laini zote zisizo na usajili kufikia Desemba 31 mwaka huu" amesema.

 Hayo ameyasema leo jijini Dar es Salaam mara baada ya kushuhudia utiwaji saini wa makubaliano ya ujenzi wa jengo la makao makuu ya umoja wa shirika la Posta Barani Afrika, Pan African Postal Union (PAPU) umoja ulio na nchi wanachama 45 na jengo hilo litajengwa jijini Arusha Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...