Meli ya MV. Nyakibalya ikiwa katika Bandari ya Bukoba mkoani Kagera.Meli hiyo ni maalumu kwa ajili ya kubeba mizigo ndani ya Ziwa Victoria.
 Meneja wa Bandari za Kanda ya Ziwa Morris Mchindiuza akizugumzia hatua mbalimbali za uboreshaji wa miundombinu katika Bandari ya Bukoba mkoani Kagera.
 Ofisa wa Bandari ya Bukoba iliyopo mkoani Kagera Bulenga Komagi akizungumza na waandish wa habari kuhusu umuhimu wa bandari hiyo kwa wananchi wa mkoa huo na nchi jirani.
 Jengo la utawala katika Bandari ya Bukoba mkoani Kagera likiwa limefanyiwa maboresho.Jengo hilo lilijengwa mwaka 1945 ambalo lilikuwa linatumiwa tangu enzi za ukoloni.




Na Said Mwishehe, Michuzi Globu -Bukoba

BANDARI ya Bukoba mkoani Kagera imetejwa kuwa miongoni mwa bandari sita kubwa zilizopo katika Ziwa Victoria ambazo zipo chini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania(TPA.

Kwa mujibu wa TPA, bandari hiyo ndio chachu ya wafanyabiashara wa Mkoa wote wa Kagera hususani  Bukoba Mjini ambao hudumia bandari kwa ajili ya kusafirisha shehena ya mizigo ya mazao ya  kilimo pamoja na bidhaa mbalimbali kwa ajili ya mahitaji ya wananchi.

Akizungumza leo Desemba 12, mwaka 2019, Meneja wa Bandari za Kanda ya Ziwa Morris Mchindiuza amefafanua  bandari hiyo ilijengwa mwaka 1945 enzi za mkoloni na baada ya uhuru ikawa chini ya Shirika la Reli na Bandari ya Afrika Mashariki mpaka ilipofika mwaka 1977 baada ya
Jumuiya ya Afrika Mashariki kuvunja ikwa chini ya Shirika la Reli Tanzania(TRC).

"Ilipofika mwaka 1997 ikawa chini ya Kampuni  ya Huduma za Meli Tanzania( MSCL) ambao kampuni hiyo waliendelea kuihudumia bandari mpaka mwaka 2004 ilipoundwa Sheria ya TPA kwa Sheria namba 17 ikawa chini ya Usimamizi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania. 

"Bandari hii ni kongwe na ilikuwa na miundombinu iliyokuwa imechakaa na hivyo TPA tukaamua kuiboresha miundombinu yake.Tunatarajia baada ya kukamilika bandari hii itarejea tena katika shughuli zake hasa kwa kutambua kuanzia mwakani meli ya MV Victoria inatarajiwa kuanza tena safari zake,"amesema.

Ameongeza mradi wa kuboresha bandari hiyo pamoja na maeneo mengine umegusa pia majengo ya  abiria ambapo kulikuwa na uboreshaji wa awamu mbili, ya kwanza ilishakamilika na awamu ya pili imekamilika hivi karibuni.

"Katika maboresho haya tumetumia gharama ya shilingi  milioni 565 kwa kazi hii ya kuhuisha jengo zima la abiria na jengo la utawala, kwa sasa hivi kila kitu kimekamilika na kwa upande wa huu.

"Pia tunaendelea na ukarabati wa majengo ya kuhifadhia mizigo ambao nao huu upo katika mradi mwingine wa uboreshaji a miundombinu ya Bandari kwa eneo la Bukoba, Kemondo, Mwanza Kaskazini na Kusini,"amesema Mchindiuza.

Ameogeza miaka ya nyuma kidogo kulikuwa na meli za MSCL ambazo zilifanyakazi ikiwamo meli ya Mv. Bukoba iliyoanzia katika bandari hiyo hadi bandari ya  Mwanza, Meli ya Mv. Victoria nayo ilikuwa ikija hapa pamoja na meli ya na Mv Serengeti. 

"Tunatarajia meli ya Mv.Victoria kuanzia mwezi wa mwakani itarudi kwenye safari zake na kubeba shehena.Kwa kipindi hiki tumekuwa tukiendelea kutoka huduma hasa kwa wateja wakubwa wawili ambao ni Kagera Sugar ambaye amekuwa akitumia bandari hii kusafirisha sukari kutoka hapa kwenda Mwanza.

"Mteja mwingine tunayemuhudumia ni mfanyabiashara Omukwano ambaye yeye amekuwa akileta bidhaa za madukani kama mafuta, sabuni kutoka nchini Uganda mpaka hapa Bukoba kwa ajili ya soko la hapa kwetu,"amesema.

Kuhusu uwezo wa bandari hiyo ameeleza imekuwa ikihudumia tani 6000 pamoja upande la jengo la abiria linauwezo wa kuwa na abiria 400 kwa wakati mmoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...