Mkurugenzi Mtendaji wa Banki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) Japhet Justine akizungumza katika Mkutano wake na Waandishi wa Habari(hawapo pichani) kuhusu Mafanikio ya Benki hiyo  katika miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Tano, Mkutano huo ulifanyika katika Ukumbi wa Idara ya Habari-MAELEZO Jijini Dar es Salaam leo Disemba 12, 2019.
Mkurugenzi Mtendaji wa Banki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), Japhet Justine akifafanua jambo  katika Mkutano wake na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu Mafanikio ya Benki hiyo katika  miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Tano, Mkutano huo ulifanyika katika Ukumbi wa Idara ya Habari-MAELEZO Jijini Dar es Salaam leo Disemba 12, 2019.
Picha na Idara ya Habari-MAELEZO
………………..

Na Mwandishi Wetu- MAELEZO
Serikali ya Awamu ya Tano Chini, Rais Dkt. John Magufuli imejikita katika kuwawezesha wakulima kwani ilitoa zaidi ya Billioni 300 kwa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania, (TADB) katika kipindi cha miaka minne ya utawala wake.

Akielezea mafanikio ya Benki hiyo katika kipindi cha miaka minne ya Serikali,  Mkurugenzi Mtendaji wa TADB Japhet Justine alisema kuwa Rais Dkt. Magufuli alitoa pesa hiyo, kwa ajili ya kusaidia sekta hiyo katika shughuli mbalimbali   ikiwemo kutoa mikopo kwa Wakulima.

‘’Katika kipindi cha miaka minne cha utawala wa Rais Dkt. Magufuli alituwezesha kutupa mtaji wa zaidi ya Sh. Billioni 300, ambapo mpaka Novemba mwaka huu, tumefanikiwa kutoa kiasi cha Sh. Billioni 148 kwa ajili ya mikopo kwa wakulima’’, alisema Bw. Justine

Justine alisema wakati wanaanzisha Benki hiyo mwaka 2016 Rais Magufuli aliwapa Billioni 60 kama mtaji, lakini  waliweza kuizungusha pesa hiyo kwa kutoa mikopo katika vyama mbalimbali vya wakulima ambapo walifanikiwa kurudisha Sh. Billioni 68 kwa muda mfupi.

Aidh Mkurugenzi huyo alisema, pesa hiyo ilijikita zaidi katika mpango wa pili wa  Maendeleo ya Kilimo, matumizi bora ya Ardhi na Maji, ambapo mpango huo ulifanikiwa na kutimiza malengo yaliyotarajiwa.

‘’Pesa hiyo ililenga zaidi katika mnyororo wa thamani wa mazao , ambapo Sh. Billioni 10 tulipeleka katika Mifugo, Billioni 1 ilienda ufugaji wa Samaki, Millioni 700 ilienda kwenye Kuku na Billioni 37 zilienda katika Mazao mbali mbali ya biashara’’, alisema Japhet.

Mkurugenzi huyo alisema, kutokana na mpango huo watu Millioni 1.6 wamefanikiwa kutokana na huduma zao hivyo katika kipindi cha miaka minne ya utawala wa Rais Magufuli Benki hiyo pamoja na wadau wake wamepata mafanikio makubwa.

Aidha Mkurugenzi huyo alisema, mbali na kutoa mikopo kwa wakulima lakini wamekuwa wakiwasaidia kutafuta  masoko hivyo inawarahisishia kuwa na uhakika wa masoko ya mazao yao.

Mkurugenzi huyo alisema katika kuimarisha kilimo na kumpa mkulima nyenzo bora, Benki hiyo imekuwa ikitoa matrekta pamoja na mashine za kuvunia mpunga kwa wakulima.Aidha Mkurugenzi huyo alisema, mbali na pesa hizo, Benki hiyo ilitoa pesa nyingine kiasi  Sh. Billioni 35 mkopo kwa Viwanda 13 vya kuchakata mazao ya Kilimo.

Japhet alitaja baadhi ya viwanda vilijengwa kutokana na mkopo huo ni pamoja na kiwanda cha Alizeti kilichopo Kahama, kiwanda cha kuchakata mafuta kilichopo Manyoni na kiwanda cha kusindika Chikichi kichopo Kigoma.

Aidha Mkurugenzi huyo alisema TADB baada ya miaka minne ya mafanikio, inatarajia kuweka nguvu zaidi na kuyaongezea thamani mazao ya Pamba na  Mkonge kwani yalikuwa yakiingiza pesa nyingi miaka ya nyuma hapa nchini.

‘’Kwakweli TADB tuna nia ya dhati ya kurudisha thamani ya zao  la Pamba na Mkonge, enzi za Mwalimu Nyerere, mazao haya yalikuwa yakiingiza pesa nyingi hapa nchini, lakini kadiri miaka ilivyosonga na mazao yalikuwa yakishuka’’, alisema.

Mkurugenzi huyo alisema Benki hiyo, inataka kufanya mapinduzi makubwa katika mazao hayo kwani wanatarajia kufufua viwanda vya kutengenezea nguo, kiwanda cha kutengeneza magunia.

Japhet amewataka Watanzania waache kuwaza kilimo cha zamani na badala yake wajiingize kwenye kilimo cha kisasa, kwani sekta hiyo hivi sasa ni biashara kubwa ambayo inawatoa watu wengi.

Mkurugenzi huyo alisema, licha ya kuwa benki hiyo kuwa na  mafaniko hayo katika kipindi cha miaka minne, lakini bado kuna changamoto ya masoko, hivyo wanatarajia kushirikiana na taasisi zilizo katika mnyororo wa thamani ndani ya Afrika Mashariki na  nchi zilizo kusini mwa Afrika (SADC) katika kutafuta masomo hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...