Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Balozi Joseph Sokoine ambaye ni mgeni Rasmiakiongea wakati wa ufunguzi wa Warsha ya mafunzo kuhusu kuhimili mabadiliko ya tabianchikwa kutumia mifumo ya ikolojia iliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais na kufanyika katikaukumbi wa Chuo cha Mipango jijini Dodoma.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira Faraja Ngereageza akiongea wakati akimkaribishaMgeni Rasmi kufungua warsha hiyo ya mafunzo kuhusu kuhimili mabadiliko ya tabianchi kwakutumia mifumo ya ikolojia iliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais na kufanyika katika
ukumbi wa chuo cha Mipango jijini Dodoma

Mgeni Rasmi katika warsha hiyo Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Balozi Joseph Sokoine akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki waliohudhuria warsha hiyo ya mafunzo kuhusu kuhimili mabadiliko ya tabia Nchi kwa kutumia mifumo ya ikolojia iliyoandaliwa na Ofisiya Makamu wa Rais na kufanyika katika ukumbi wa chuo cha Mipango Dodoma.

Meneja wa Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya tabianchi kwa kutumia Mifumo Ikolojia Vijijini Bwana George Kafumu akitoa maelezo mafupi kuhusiana na mradi huo pamoja na lengo warsha hiyo iliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais na kufanyika jijini Dodoma.
**********************************
Mifumo ikolojia yenye afya ndio inaweza kutupatia huduma za uhakika kama chakula, maji safi na salama, kutuepusha na magonjwa, mafuriko, uharibifu wa ardhi na wakati huo huo kutuwezesha kuhimili athari zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi.
Hayo yamesemwa na Naibu Katibu kuu Ofisi ya Makamu wa Rais Balozi Joseph Sokoine ambaye alikua mgeni rasmi katika ufunguzi wa warsha ya mafunzo kuhusu kuhimili mabadiliko ya tabia Nchi kwa kutumia mifumo yaikolojia iliyofanyika katika ukumbi wa chuo cha Mipango jijini Dodoma.
Alisema kuwa Kukosekana kwa huduma hizo kutapelekea kushindwa kufikia malengo ya maendeleo ya milenia (Sustainable Development Goals). Hivyo mradi huu umekuja wakati muafaka wakati pia Serikali ikiendelea kukuza uchumi katika njia endelevu.
“Kama mnavyo fahamu mabadiliko ya tabianchi yameleta athari mbalimbali kwenye mazingira yetu hapa nchini. Kati ya madhara hayo ni kuharibika kwa kanda za Ikolojia Kilimo (Agro Ecolojical Zones) ambazo kwa mujibuwa tafiti kanda hizi ziko saba. Tafiti zinaonyesha kwamba ni rahisi kuhimili (Adaptation) kuliko kukabili (Mitigation)”. Alifafanua Balozi Sokoine.
Akimkaribisha Mgeni Rasmi Kaimu Mkurugenzi wa Mazingira Bwana Faraja Ngerageza alisema kuwa warsha hiyo itawawezesha washiriki kufahamu zaidi kuhusiana na kuhimili mabadiliko ya tabia nchi kwa kutumia mifumo ya ikolojia iliyopo vijijini.
Warsha hiyo ya mafunzo ya siku tatu imeandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais kupitia mradi wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi kwa kutumia mifumo ya ikolojia vijini (EBARR). Mradi huu unatekelezwa na Ofisi yaMakamu wa Rais. Warsha hiyoimehudhuriwa na Washiriki kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali, inafanyika katika ukumbi wa Mikutano wa chuo cha Mipango jijini Dodoma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...