Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

RAIS wa zamani wa Pakistan, Pervez Musharraf (76) amehukumiwa kifo katika kesi ya Uhaini mkubwa iliyohusisha kuweko kwa dharura ya Kikatiba nchini humo mnamo mwaka  2007.

 Wakati wa hali ya dharura, Mahakama kuu haikupitisha hili hivyo Pervez aliamrisha kukamatwa na kuteswa kwa wanasiasa na mawakili ambao walikuwa kinyume na yeye.

Jumanne ya Desemba 17, amehukumiwa kwa mashtaka hayo katika mahakama kuu mjini Islamabad na kuweka historia nchini humo kwa kuwa kiongozi wa kwanza wa kijeshi kuhukumiwa akiwa madarakani.

Baada ya kuondolewa madarakani na jeshi hilo mwaka 1999, hadi sasa jeshi la nchi hiyo linaendelea kudhibiti masuala ya usalama, ulinzi pamoja na sera za ndani na nje ya nchi.

Aidha Chama cha uislamu cha Musharraf's  All Pakistan Muslimu League (APML) kimeeleza kuwa watakata rufaa mapema, huku ikinukuliwa kuwa kuwa Musharraf alienda nchi za kiarabu 2016 na kukataa kuhudhuria  na kujitetea juu ya kesi iliyokuwa inamkabili na aliondoka nchini humo na kwenda Dubai kwa matibabu na video iliyochukuliwa kutoka hospitali hapo imeonesha kuwa aliruhusiwa mapema mwezi huu.

Hadi hukumu hiyo inatolewa kiongozi huyo akiwa Mjini Dubai tangu alipoondoka Machi 2016 kwasababu za Kiafya. Musharraf alitolewa madarakani mwaka 1999 kwa mapinduzi ya kijeshi.

Tusisahau, Bado anahusishwa na Mauaji ya Benazir Bhutto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...