Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni leo tarehe 18/12/2019 amehitimisha
maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wahamaji katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja
vya Uhamiaji Kurasini Dar Es Salaam. Maadhimisho hayo ambayo yanafanyika kila
mwaka yanalenga kutambua haki za wahamaji pamoja na familia zao wanapokuwepo
katika nchi za kigeni.
Akihutubia
katika Maadhimisho hayo Mheshimiwa Masauni amempongeza Kamishna Jenerali wa
Uhamiaji Dkt. Anna Makakala kwa kufanya mabadiliko makubwa kwenye Mifumo ya
kutolea huduma zake kwa njia ya Mtandao ambapo sasa mgeni anaweza kuomba Visa
au Vibali vya Ukaazi, kufanya malipo pamoja na kupokea kibali chake kwa njia ya
mtandao akiwa mahali popote Ulimwenguni bila ya kulazimika kufika katika Ofisi
za Uhamiaji.
Aidha,
Naibu Waziri aliongeza kuwa Serikali imefanya marekebisho ya Sheria ya Uhamiaji
kwa kuanzisha vibali maalumu vya ukaazi kwa wahamiaji walowezi walioo hapa
nchini ili kutatua tatizo la uhamiaji haramu nchini. Pia Serikali imepunguza
ada ya kibali cha Ukaazi kwa wawekezaji wan je wenye asili ya Tanzania
(Diaspora) kutoka Dola za Kimarekani 3050 hadi kufikia Dola 1000 ili
kuhamasisha raia hao kuwekeza katika nchi yao ya asili.
Awali
akimkaribisha Naibu Waziri Masauni, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna
Makakala ameeleza kuwa kwa sasa Idara ya Uhamiaji inaendelea kuzifanyia kazi
changamoto zinazo wakabili wateja wa huduma za Uhamiaji.
Dkt.
Makakala aliongeza kuwa kutokana na maboresho hayo, Waombaji wa huduma za
Uhamiaji hususani Pasipoti
hawatalazimika kuwasilisha katika Ofisi za Uhamiaji Viambata vya nakala halisi
watakapo hitaji Pasipoti. Badala yake Viambato hivyo vitatakiwa kuwasilishwa
kwa njia ya Mtandao pekee.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...