Meneja Ukuzaji wa Biashara wa NBC, Jonathan Bitababaje akichangia mada wakati wa semina ya siku moja iliyoandaliwa na Benki hiyo ya wafanyabiashara wadogo na wa kati kwa lengo la kuwawezesha kimafunzo kuhusu ukuaji wa biashara zao  jijini  Dar es Salaam juzi.

 Baadhi ya washiriki wa semina hiyo wakisikiliza kwa makini baadhi ya mada zilizokuwa zikitolewa katika Semina hiyo kutoka wadau mbalimbali wakiwemo Mamlaka ya Mapato (TRA), Wakala wa Usajili wa Biashara na Makampuni (Brela), Chemba ya Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA),  Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) pamoja na wengineo.

Baadhi ya wafanyabiashara wa maeneo ya Ubungo jijini Dar es Salaam wakisikiliza baadhi ya watoa mada katika semina iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa ajili ya wafanyabiashara hao juzi. 
Msaidizi wa Msajili Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), George Chuwa akizungumza wakati semina ya siku moja iliyoandaliwa na benki ya NBC kwa wateja wake wafanyabiashara wadogo na wa kati wa maeneo ya Ubungo jijini Dar es Salaam jana.

 Mkurugenzi wa Bima wa Benki ya NBC, Benjamin Nkaka (kulia) akisalimiana na wafanyabiashara wadogo na wa kati wa maeneo ya Ubungo katika semina ya siku moja ilyoandaliwa na benki hiyo kwa lengo la kuwawezesha kimafunzo kuhusu ukuaji za mbinu za kufanya biashara zao  jijini  Dar es Salaam jana.
 Meneja wa Kanda ya Dar es Salaam wa Benki ya NBC, Rachel Mwalukasa (kulia), akizungumza na wafanyabiashara wa maeneo ya Ubungo jijini humo jana kuhusu huduma na bidhaa zotolewazo na benki hiyo hususani wakati wa semina iliyoandaliwa na benki hiyo kwa kushirikiana na wadau muhimu kutoka taasisi mbalimbali zinazuhusika na masuala ya biashara.
 Mwakilishi kutoka Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Gwakisa Bapala (kulia), akizungumzia shughuli mbalimbali zinazofanywa na baraza hilo wakati wa semina kuhusu mbinu mbalimbali za kufanya biashara iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati katika Ukumbi wa Hoteli ya Millenium Towers jijini Dar es Salaam juzi.
 Mkuu wa Kitengo cha Wafanyabiashra wa Kati na Wadogo wa Benki ya NBC, Evance Luhimbo akizungumza katika semina ya siku moja ya  wafanyabiashara wadogo na wa kati wa maeneo ya Ubungo  iliyoandaliwa na benki hiyo kwa lengo la kuwawezesha kimafunzo kuhusu ukuaji wa biashara zao  jijini  Dar es Salaam juzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...