Wamiliki wa viwanda mkoa wa Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu uwekezaji,Mhe Angela Kairuki wakati akifanya ziara ya kutembelea viwanda mkoani morogoro orogoro walalmikia sheria ya ushuru wa forodha ya East Africa sambamba na VAT  kukwamisha ukuaji wa viwanda  vya ndani hali inayo fanya washindwe kushindana na viwanda vya nje ya nchi.

Wamiliki hao wameeleza changamoto hizo mbele ya Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu uwekezaji,Mhe Angela Kairuki wakati akifanya ziara ya kutembelea viwanda mkoani Morogoro na kujua changamoto zao sambamba na namna gani ya kutatua.

Aidha badhi ya changamoto zilizo lalamikiwa ni pamoja na sheria ya ushuru ya Afrika Mashariki zinazo daiwa kutoa nafuu kwa bidhaa za nje hali inayopelekea viwanda vya ndani kushindwa kushindana  na wengine wakabainisha changamoto ya vat kuwa juu pamoja na malipo ya osha kuwa ni kikwazo kikubwa.

Hali hiyo wameeleza kuwa imewafanya wapate woga kwa wawekezaji kwa kuhofia kushindwa kufanya biashara nchini na kupelekea nchi kuendelea kuagiza nguo na vitu mbalimbali kutoka nje ya nchi.
 
kwa upande wake Waziri Kairuki amewahakikishia Wawekezaji hao kuwa Serikali imeyapokea yote na kujiandaa kuzifanyia kazi mapeMa changamoto zao,  ambapo ameahidi kushirikisha Mawaziri wote husika katika kupitia kanuni na miongozo mbali mbali ili kurekebisha
 Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu uwekezaji,Mhe Angela Kairuki akikagua moja ya kiwanda wakati akifanya ziara ya kutembelea viwanda mkoani morogoro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...