Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na Waheshimiwa Wabunge, wageni waalikwa wakati wa Mkutano wa Viongozi kuhusu familia yenye baraka tukio lililofanyika leo katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam.

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akionyesha tuzo maalum ya udumishaji wa amani aliyopatiwa leo katika Mkutano wa viongozi kuhusu familia yenye baraka tukio lililofanyika katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Universal Peace Foundation Bara la Afrika, Rev. Bakary Camara na kushoto ni Mbunge wa Sengerema, Mhe. William Ngeleja

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kushoto) akizungumza na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj Mussa Salum (kushoto) walipokutana leo katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam. Kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Viongozi kuhusu familia yenye baraka, Wa pili kushoto ni Mbunge wa Igagula, Mhe. Mussa Ntimizi na Mbunge wa Sengerema, Mhe. William Ngeleja.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...