Picha ya viongozi wa mitaa kata ya  Olasiti na wataalam wakiwa katika wakiwa katika mtaa wa Oleresho pamoja na maafisa kutoka Tanesco ambapo walipitia kuhakiki kaya zisizokuwa na umeme. 
Na Vero Ignatus,Arusha.
Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo  kwa 
Shirika la umeme Tanesco limeanza kutekeleza agizo la mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ambalo aliwataka kuwaunganishia umeme kaya zaidi ya 200 zilizopo katika kata ya Olasiti ,baada ya Kamati ya Maendeleo ya Kata hiyo ikiongozwa na Diwani na Afisa Tarafa ya Elerai  pamoja na Wataalamu wa Tanesco kufanya ziara ya kupima maeneo na kufanya zoezi la kubaini kaya hizo ili kuziunganishia na umeme.
Alex Martinni diwani wa  wa Kata ya Olasiti  alisema watahakikisha kuwa agizo hilo linatekelezwa ambapo wamewatembeza wataalamu kutoka Tanseco ili waweze kujionea  kaya hizo zilizoko katika mtaa wa Oleresho na Kimindoros ambazo licha ya kuwa ndani ya jiji la Arusha hazina huduma ya umeme.
Martin  ameipongeza serikali kwa kusikia kilio cha muda mrefu cha wananchi na kuagiza wananchi hao waunganishe na huduma ya umeme ambayo ni kichocheo cha maendeleo kwa wananchi na jamii kwa ujumla.
Afisa Tarafa wa Elerai Titho Cholobi amesema kuwa wataalamu hao wameanza kupima maeneo na hatua inayofuata ni kuweka nguzo na kusogeza umeme  tayari kwa ajili ya kuwaunganishia wananchi.
Cholobi amesema kuwa kufika kwa Wataalamu hao wa Tanesco ni  utekelezaji wa Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo alipofanya ziara yake katika kata hiyo na kusikiliza kero za wananchi ambapo aliwataka Tanesco kufika katika kata hiyo na kuwauganisha wananchi na huduma ya umeme.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Oleresho Elia Kayan  amesema kuwa wanatarajia kaya nyingi zitanufaika na huduma ya umeme licha ya kukaa muda mrefu bila kupata huduma ya umeme.
Amesema kuwa serikali imetoa agizo hilo kutokana na kutambua changamoto za wananchi hao hivyo wananchi wapo tayari kushirikiana na Wataalamu katika kutekeleza agizo hilo.
''Tumeanza kuwahamasisha wananchi kuandaa nyumba zao na kuweka mifumo ya kuingiza umeme ili umeme huo ukifika karibu na makazi yao kusiwe na vikwazo vyovyote" Alisema Mwenyekiti huyo

Mtaalamu kutoka Tanesco Idara ya Upimaji aliyejitambulisha kwa jina la Elia amesema kuwa tayari wamejionea hali halisi na kuwataka Wenyeviti wa mtaa kufanya vikao na kukubaliana njia ambazo umeme utapita ili kuepuka migogoro isiyo ya lazima katika utekelezaji wa agizo hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...