Na Editha Edward, Michuzi TV, Tabora 

Mkuu wa mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri amewasisitiza wafungwa Walionufaika na Msamaha wa Rais ya jamhuri ya muungano wa Tanzania alioutoa hapo jana katika maadhimisho ya miaka 58 ya uhuru kuwa wautumie Msamaha wa Rais kwa kutenda mema katika jamii wanazoenda kujumuika nazo kwani walipokuwa katika magereza hayo walijifunza mafunzo mbalimbali ikiwemo useremala ujenzi uashi kilimo poa walijifunza heshima na maadili hivyo ni vyema kuutumia vizuri Msamaha hyo

Mkuu wa gereza la uyui Omary Tensen amesema wafungwa hao Walionufaika kwa Msamaha wa Rais hapo jana kwa pamoja amewataka kuhakikisha hawarudi kufanya makosa hivyo wautumie fursa Hiyo kufanya kazi kwa bidii katika jamii zao ili kujikimu kiuchumi

Sonda Deus ambae ni miongoni mwa wanufaika wa Msamaha wa Rais amesema anamshukuru mhe, Rais Magufuli kwa kuwakumbuka walioko magerezani na anafurahi kuachiwa huru na  kwenda kuungana na familia yake. 
Mkuu wa mkoa wa Tabora Mhe. Aggrey Mwanri akizungumza leo na wafungwa walionufaika na Msamaha wa Rais alioutoa jana katika maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru.

 Mkuu wa gereza la uyui Omary Tensen akizungumza na wafungwa Walionufaika na Msamaha wa Rais

Baadhi ya wafungwa Walionufaika na Msamaha wa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania wakiwa nje ya gereza tayari kwenda makwao

Gereza kuu la Uyui la Mkoani Tabora

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...