Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

WANANDOA Kenneth na Mary Odipo waliofunga ndoa ya kifahari wiki moja iliyopita huko Kisumu nchini Kenya wamejiua kwa kile kilichoelezwa ni mzigo wa madeni uliokuwa ukiwaandama ukiwemo moja ya Benki DTB kutaka kuuza nyumba ya wanandoa hao iliyopo Nyakenda Estate ili kufidia deni.

Mtandao wa Kenya Today umeripoti kuwa wanandoa hao walijiua siku nne tuu mara baada ya harusi yao na ni baada ya kugundua kuwa deni ambalo limetokana na harusi limefikia shilingi ya Kenya 7.9 milioni ambayo ni sawa na dola za kimarekani 78,000 na shilingi za kitanzania milioni 170.

Imeripotiwa kuwa kabla ya kutoa uhai wao waliacha ujumbe ulisomeka; 
"Tumedharirika na kuona aibu kuwa hatuwezi kuanza maisha yetu kwa furaha kwa kuwa ninyi (watu) hamjatufurahisha kama tulivyotegemea" ulisomeka ujumbe huo.

Imeelezwa kuwa wanandoa hao wametoa lawama kwa wageni waalikwa ambao walihudhuria harusi hiyo na kula bila kuja na zawadi hali iliyopelekea kushindwa kwenda kwenye fungate kama walivyopanga.

Imeelezwa kuwa harusi hiyo ilifanyika katika hoteli ya nyota tano na kualikwa watu wa hadhi ya juu waliotegemewa wangetoa zawadi za thamani na Fedha nyingi.

Vilevile imeelezwa kuwa kifo hicho ambacho kimegusa familia zote mbili, katika siku ya  harusi hiyo helikopta tatu zilikodiwa kubeba wanafamilia na maharusi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...