KITUO cha ujasiriamali cha CEED Tanzania, kimetoa mafunzo ya uendeshaji na usimamizi wa biashara kwa wajasiriamali mkoani Morogoro yenye lengo la kuwawezesha namna ya kusimamia biashara zao, kushirikiana pamoja katika kutatua changamoto za kibiashara pamoja na fursa mbalimbali mkoani humo.
Akizungumza na wajasiriamali wa mkoani Morogoro, Bw Atiba Amalile ambaye ni Mkurugenzi wa CEED Tanzania, amewakumbusha wajasiriamali hao kuwa haitakuwa biashara kama kawaida ikiwa Tanzania itakuwa nchi ya kipato cha kati miaka ijayo.
Naye Bwana Baptist Mnyalape ,mshauri wa masuala ya kodi na mwakilishi wa CEED Tanzania jijini Dodoma amewahimiza wajasiriamali wa Morogoro kuhakikisha wanafahamu kanuni zinazoweza kuathiri biashara zao moja kwa moja.
‘’ Niwakumbushe tu ndugu zangu wajasiriamali kuhusu kuzingatia masuala mazima ya kodi, tuhakikishe tunafahamu kanuni na sheria ambazo zinaweza kuingilia na kuathiri biashara zetu moja kwa moja, ukishindwa kuzingatia haya itagharimu muda wako pamoja na pesa zako," Amesema Mnyalape.
Kwa upande wa mwakilishi kutoka Benki ya CRDB, Dennis Kayanda amewasisitizia wajasiriamali hao juu ya umuhimu wa kufuata sheria ya matumizi ya ushuru wa ardhi na kusema ni hatari zaidi kwa kutafuta mikopo kutoka benki za biashara na kuwekeza katika biashara ambazo zinaweza kuwa hazifanyi kazi katika eneo hilo na hivyo kuathiri biashara.
Naye Bwana Victor Mfinanga mnufaikaji wa mafunzo hayo na Mkurugenzi Mtendaji wa Maziwa Shambani Milk mkoani Morogoro amefurahia kupata nafasi tena kwani mafunzo haya yamemuwezesha kufahamu namna ya kuendesha biashara yake.
‘‘Nimekuwa nikihudhuria mara kwa mara mafunzo ya CEED, mfano mafunzo yaliyokuwa yakitolewa jijini Dar es Salaam na CEED Tanzania yamenisaida kujua habari za biashara bora, namna ambavyo mtu unawezakutumia teknolojia kujifunza namna ya kuendesha biashara yako," Amesema Mfinanga.
Mafunzo hayo yameudhuriwa na wajasiriamali mbalimbali wa mkoani Morogoro na wawakilishi kutoka benki za CRDB, NMB NBC, Azania, pamoja na Benki ya Afrika ambazo kwa pamoja zimewapa elimu wajasiriamali jinsi ya kupata mikopo bila shida na namna ya kutumia mikopo hiyo kukuza biashara zao.
Akizungumza na wajasiriamali wa mkoani Morogoro, Bw Atiba Amalile ambaye ni Mkurugenzi wa CEED Tanzania, amewakumbusha wajasiriamali hao kuwa haitakuwa biashara kama kawaida ikiwa Tanzania itakuwa nchi ya kipato cha kati miaka ijayo.
Naye Bwana Baptist Mnyalape ,mshauri wa masuala ya kodi na mwakilishi wa CEED Tanzania jijini Dodoma amewahimiza wajasiriamali wa Morogoro kuhakikisha wanafahamu kanuni zinazoweza kuathiri biashara zao moja kwa moja.
‘’ Niwakumbushe tu ndugu zangu wajasiriamali kuhusu kuzingatia masuala mazima ya kodi, tuhakikishe tunafahamu kanuni na sheria ambazo zinaweza kuingilia na kuathiri biashara zetu moja kwa moja, ukishindwa kuzingatia haya itagharimu muda wako pamoja na pesa zako," Amesema Mnyalape.
Kwa upande wa mwakilishi kutoka Benki ya CRDB, Dennis Kayanda amewasisitizia wajasiriamali hao juu ya umuhimu wa kufuata sheria ya matumizi ya ushuru wa ardhi na kusema ni hatari zaidi kwa kutafuta mikopo kutoka benki za biashara na kuwekeza katika biashara ambazo zinaweza kuwa hazifanyi kazi katika eneo hilo na hivyo kuathiri biashara.
Naye Bwana Victor Mfinanga mnufaikaji wa mafunzo hayo na Mkurugenzi Mtendaji wa Maziwa Shambani Milk mkoani Morogoro amefurahia kupata nafasi tena kwani mafunzo haya yamemuwezesha kufahamu namna ya kuendesha biashara yake.
‘‘Nimekuwa nikihudhuria mara kwa mara mafunzo ya CEED, mfano mafunzo yaliyokuwa yakitolewa jijini Dar es Salaam na CEED Tanzania yamenisaida kujua habari za biashara bora, namna ambavyo mtu unawezakutumia teknolojia kujifunza namna ya kuendesha biashara yako," Amesema Mfinanga.
Mafunzo hayo yameudhuriwa na wajasiriamali mbalimbali wa mkoani Morogoro na wawakilishi kutoka benki za CRDB, NMB NBC, Azania, pamoja na Benki ya Afrika ambazo kwa pamoja zimewapa elimu wajasiriamali jinsi ya kupata mikopo bila shida na namna ya kutumia mikopo hiyo kukuza biashara zao.
Mmoja wa wanachama wa CEED Tanzania na Mkurugenzi wa Shambani Milk, Victor Mfinanga akielezea namna ambavyo amenufaika na elimu za ujasiriamali na kutoa wito kwa wafanyabiashara wadogo kuwa na utaratibu wa kujifunza
Balozi wa CEED Tanzania, Dennis Kayanda akiwafundisha wajasiriamali mkoani Morogoro njia bora za ufanyaji wa biashara
Washiriki mbalimbali wa mafunzo ya ujasiriamali wakifuatilia mafunzo hayo kutoka kwa wawezeshaji. Mafunzo hayo yamefanyika kwa wajasiriamali mkoani Morogoro.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...