Na  Mwandishi Wetu
Wakala wa Vipomo Nchini (WMA) imesema kuwa itaendelea kulinda maslahi yawatumiaji na afanyabiashara kupata stahiki sahihi katika manunuzi na uuzaji wabidhaa zao kwa kutumia vipimo vinavyoendana na thamani ya pesa inayolipwa na mteja.

Akizunngumza Jijini Dar es Salaam katika ziara ya Kustukiza kwa Wafanyabiashara wa Mabucha, Kaimu Meneja wa Wakala wa Vipimo Mkoa wa Temeke, Krishna Mahamba amesema kuwa dhumuni la ziara hiyo ni kuangalia kama vipimo vinazingatiwa na wauzaji ili kuleta usawa kwa wateja na wauzaji hao.

“Katika kuadhimisha miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika, Wakala wa Vipimo leotumeamu kufanya zoezi hili ambalo linafanyika Nchi nzima ili kulinda haki zabiashara kwa wateja na wauzaji kwenye mabucha haya, kwani mara nyingi katika siku za sikukuu kama hizi wauzaji huwa wanachezea vipimo”, Krishna Mahamba Kaimu Meneje (WMA) Mkoa wa Temeke.

Alieleza kuwa wafanyabiashara wa mabucha wanapaswa kutumia mizani
iliyopimwa ili kumuwezesha mpata huduma katika mabucha yao kupata bidhaa kulingana na thamani ya pesa yake na kuweza kuleta usawa pande zote mbiliyaani mteja na muuzaji.

Naye Kaimu Meneje Wakala wa Vipimo Mkoa wa Kinondoni, Charles Mavundealisema kuwa leo wakala wa vipimo imefanya zoezi hilo ili kuangalia kamawafanyabiashara wa Mabucha wanazingatia Sheria ya Vipimo nchini Sura namba340 ambayo inamtaka mfanyabiashara kutumia vipimo sahihi kulingana na bei ya bidhaa yake aliyoipanga kwa wanunuzi.

Mavunde alito wito kwa watanzania kuwa wanapokuwa wanaadhimisha sikukuukama ilivyokuwa leo miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika wawe makini nawafanyabiashara katika sehemu zote za biashara kuanzia kwenye mabucha, sokoni na kwenye vituo vya mafuta kwa kuwa siku hizo wafanyabiashara huchezea vipimo na kutoa bidhaa kwa kuwapunja wateja wao.

Kwa upande wake, Meneja Mawasiliano kutoka (WMA), Irene John alisema kuwawakala wa vipimo hawajalala katika siku za sikukuu, wataendelea kufanya ziara za kustukiza kwenye sehemu mbalimbali za biashara ikiwemo kwenye mabucha,sokoni na Vituo vya mafuta ili kuleta usawa kati ya Muuzaji na Mteja kupata stahiki zao kulingana na thamani ya pesa inayolipwa.
“Katika Maadhimisho haya ya Miaka 58 Uhuru Tanganyika hatujalala tumefanyazoezi la ukaguzi wa kustukiza kwenye mabucha hapa Mwenge Jijini Dar es Salaam na zoezi hili linafanyioka nchi nzima, na lengo kuu ni kulinda stahiki za wateja na wauzaji ili kila mtu akitoa pesa ya lita moja apate lita moja, akitoa pesa ya kilo moja vilevile apate kilo moja”, Irene John Meneja Mwasiliano (WMA).
Kaimu Meneja Wakala wa Vipimo Mkoa wa Temeke, Bw.Krishna Mahamba,
akieleza jambo kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu umuhimu wa kutumia mizani iliyosawa kwa wauzaji wa mabucha , mara baada ya Kufanyaukaguzi wa Kustukiza katika mabuchani yaliyoko Mwenge Jijini Dar es Salaammapema leo Desemba 09, 2019.
Mmoja ya Wauzaji wa mabucha yaliyoko Mwenge Jijini Dar es Salaam, Petro
Makole, akieleza jambo kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu
umuhimu wa kutumia mizani iliyosawa kwa wauzaji wa mabucha , mara baada ya Kufanyiwa ukaguzi wa Kustukiza buchani kwake Mwenge Jijini Dar es Salaam mapema leo Desemba 09, 2019. Afisa Vipimo namba Moja kutoka Wakala wa Vipimo nchini, Bw.Mohammed
akitoa maelezo kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu matumizi yakifaa cha kupimia vipimo vya kuuzia nyama, mara baada ya Kufanya ukaguzi waKustukiza katika mabucha ya Mwenge Jijini Dar es Salaam mapema leo Desemba09, 2019.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...