Na.Khadija seif, Michuzi TV

MLEZI wa kituo cha kulea watoto yatima cha kurasini Bi.Anna amewaomba wazazi kuiona fursa ya kusaidia watoto waishio kwenye mazingira magumu

Bi.Anna amesema hayo wakati wa sherehe ya kukaribisha sikukuu ya krismas iliyoandaliwa na hoteli ya serena jijini Dar es salaam na kujumuisha watoto yatima kutoka vituo mbalimbali .

"Watoto hawa ni wetu sote jukumu la kuwalea sio la serikali au watu binafsi peke yao bali ni jukumu la Kila mtanzania kwani tukiwaacha  tunawatengenezea mazingira hatarishi na kupelekea kujiingiza kwenye vitendo viovu vya ubakaji,ukahaba pamoja wizi na kusababisha nchi kuwa na watu waovu wengi na kurudisha maendeleo ya jamii yetu kuzorota"

Aidha,mama mlezi wa watoto ameeleza changamoto anazopitia katika ukuaji wao hasa wale walemavu ni pamoja na kukosa vifaa vinavyowawezesha kufanya mawasiliano ya usiku kwa viziwi, na baiskeli kwa watoto walemavu wa miguu.

"Kuelekea sikukuu ya Christmas na sikukuu nyingine watu wamekua wakija kituoni na kuwapatia misaada mbalimbali watoto wetu kuonyesha upendo na jinsi gani wanawathamini watoto ,"

Pia amewapongeza uongozi wa hoteli ya serena kwa kuendelea kuonyesha upendo wa dhati kila mwaka na kuwakaribisha watoto na kucheza,kujumuika kwenye chakula pamoja nao.

''watoto wanapokutana na kushiriki michezo inawajengea uwezo wa kujiamini mbele za watu na pia inatupa uhalisia kuwa hata wao wanavipaji vingi na hasa leo tumeona wengi wanajua kuimba na kucheza,"
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...