


…………………………………………………..
Na Farida Ramadhani na Saidina Msangi WFM, Dodoma
Wizara ya Fedha 
na Mipango imeahidi kufanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na wataalamu 
wa mipango ili kuboresha usimamizi wa sera na mipango ya maendeleo ya 
nchi.
Hayo yameelezwa 
na Kamshina wa Sera wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. William Mhoja 
wakati wa kuhitimisha kongamano la Wanamipango kwa mwaka 2019 
lililofanyika Jijini Dodoma.
Bw. Mhoja alisema
 kuwa kongamano hilo limetoa mapendekezo muhimu ambayo yatasaidia 
kuboresha upangaji na utekelezaji wa sera na mipango mbalimbali ya 
maendeleo nchini.
Aliwashukuru 
washiriki wote kwa michango, mawazo na fikra pevu wakati wa kongamano 
ambayo itasaidia katika kutatua changamoto mbalimbali zinazohusu taaluma
 ya mipango.
Naye Mchumi Mkuu 
Wizara ya Kilimo Bw.Adam Msumule ,ambaye ni miongoni mwa washiriki wa 
kongamano hilo amepongeza waandaaji wa kongamano hilo muhimu kwa ajili 
ya kubadilishana uzoefu na kuboresha mipango ya nchi.
Bw. Msumule 
alishauri kongamano hilo kufanyika kila mwaka ili kutoa fursa kwa 
wataalamu kufanya tathmnini ya mipango iliyopo, iliyotekelezwa na kuona 
namna ya kuiboresha.
Kongamano hilo 
lililokuwa na kauli mbiu ugharamiaji wa maendeleo, lilitoa fursa kwa 
washiriki kujadili mawasilisho mbalimbali ikiwemo vyanzo bunifu vya 
ugharamiaji mipango ya maendeleo ya Taifa, Sera, Sheria na mfumo wa 
kitaasisi unaosimamia ugharamiaji wa maendeleo nchini.


 

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...