Maafisa wa Wizara wakiwa ndani ya Banda la Wizara tayari kwa ajili ya kuwahudumia wananchi watakaotembelea Maonesho ya Nne ya Viwanda yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Ukuzaji Biashara Tanzania (TANTRADE) yaliyoanza tarehe 5, Desemba 2019 katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam.
Maafisa wa Wizara wakiwa ndani ya Banda la Wizara tayari kwa ajili ya kuwahudumia wananchi watakaotembelea Maonesho ya Nne ya Viwanda yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Ukuzaji Biashara Tanzania (TANTRADE) yaliyoanza tarehe 5, Desemba 2019 katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam.
Afisa wa Wizara akiwa ndanii ya Banda la Wizara tayari kwa ajili ya kuwahudumia wananchi watakaotembelea Maonesho ya Nne ya Viwanda yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Ukuzaji Biashara Tanzania (TANTRADE) yaliyoanza tarehe 5, Desemba 2019 katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam.

………………

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inashiriki katika Maonesho ya Nne ya Viwanda yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE).

Kupitia Maonesho hayo, Wananchi wanaelimishwa kuhusu majukumu ya Wizara na utekele zaji wake na namna wizara na balozi za Tanzania zinavyofanya kazi ya kuvutia watalii na wawekezaji kuja nchini kutembelea vivutio vya kitalii na kuwekeza nchini.

Maonesho hayo ni utekelezaji kwa vitendo kwa azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kujenga Uchumi wa Viwanda ili kufikia malengo ya Dira ya Maendeleo ya Taifa 2021.

Kauli mbiu ya maonesho hayo ya Tanzania sasa Tunajenga Viwanda inalenga kujenga na kuimarisha utamaduni wa Watanzania kutambua, kununua na kuthamini bidhaa zinazozalishwa nchini.

Maonyesho ya Nne ya Viwanda yanahusisha wadau wa Sekta ya Viwanda na yataonesha fursa zilizopo katika katika sekta ya viwanda na yatatoa fursa kwa wadau kuzungumza na kujadili namna ya kujenga mahusiano endelevu ya biashara.

Maonyesho hayo pia yatawezesha kufanyika kwa mikutano ya wafanyabiashara ambayo itawakutanisha wauzaji na wanunuzi .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...