Serikali imewataka watanzania kuwa watulivu, makini na kupenda kuwa na subira ya kupata maelezo,maelekezo na ufafanuzi rasmi wa Serikali pale kunakotokea jambo badala ya kukimbilia kwenye mitandao na uvumi ili kuondoa kueneza hali ya taharuki kwa wananchi bila ya kuwa na uhakika.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi ameyasema hayo wakati akitoa ufafanuzi juu ya hali ya Watanzania waishio nchini China kutokana na kuzuka kwa virusi vya homa ya corona nchini humo.

Prof. Kabudi amesema Tanzania ina wanafunzi takribani 4000 ambapo katika mji wa Wuhan kuna wanafunzi 400 na kwamba kwa mujibu wa Balozi wa Tanzania Nchini China Balozi Mbelwa Kairuki ameihakikishia serikali kuwa mpaka sasa hakuna mtanzania yeyote aliyeathiriwa ama kukumbwa na maradhi hayo.

Ameongeza kuwa Tanzania inaendelea kufuatilia kwa ukaribu kujua maendeleo na hali za watanzania wanaoishi jimboni Wuhan na China kwa Ujumla.

Aidha amewataka Watanzania kuwa makini na suala la kutoa taarifa zisizo rasmi ama uvumu kwani kwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria za Tanzania na kuwataka kuwa na Subira kupata taarifa rasmi kutoka serikalini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...