Na Nyamiti Kayora Dar es salaam

MKUFUNZI kutoka mtandao wa Jinsia na nishati endelevu Tanzania (TANGSEN) Thabit Mikidadi, amesema moja ya sababu inayopelekea matatizo ya ubakaji ni ukosefu wa nishati ya kupikia majumbani hususani vijijini.

Alisema watu wa nishati wanaamini moja ya matatizo ya kijinsi, ikiwemo ubakaji yanaweza kusababishwa na ukosefu wa nishati muhimu ikiwemo Kuni.

Thabiti aliyaeleza hayo wakati akieleza kazi,  majukumu na dhamira ya TANGSEN, kwa waandishi wa habari wa za mazingira na nishati jadidifu nchini Tanzania, kuingiza masuala ya jinsia katika sekta ya nishati, mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salam.

Alisema suala la nishati ni kitu muhimu katika sekta zote, hivyo waandishi wa habari watakapoweza kuripoti vizuri habari za jinsia, katika nishati kunaweza kutokea mabadiliko makubwa nchini.

“Sisi watu wa nishati tunasema moja wapo ya matatizo ya kijinsia, kama ubakaji yanaweza kusababishwa na ukosefu wa nishati, ni vizuri waandishi kutumia kalamu zenu katika kuandika habari zenu”alisema.

Kwa upande wake Caroline Gilbert kutoka mtandao wa Solar Sister Tanzania, alisema zaidi ya wajasiriamali 4000 wamehamasiaka kufanya biashara za sola, ambapo kwa Afrika watu Milioni 1.5 wanatumia nishari safi.

Alisema asilimia 75%wananchi wa Afrika wanaoishi vijijini bado wanategemea mwanga wa umeme wa sola, ambapo asilimia 26% ya wanawake wamejiingiza katika bishara za ujasiriamali huku wakitegemewa nishati mbadala.

Alifahamisha kuwa kumekuwa na vyanzo mbali mbali vya kupata mwangaza, vimekuwa ni hatari kwa mazingira na afya ya watumiaji, hivyo wananchi wanapaswa kuwa makini wakati wa ununuzi wa vitu hivyo.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Nukta Africa Tanzania, Nuzulack Dausen, alisema mafunzo kwa   waandishi wa habari yanalenga kujifunza mambo mbali mbali ya msingi katika kuripoti habari za nishati Jadidifu.

Alisema waandishi wameweza kujua mbinu mbali mbali za kisasa, katika kuripoti habari kwa kutumia Takwimu, kutokana na mabadiliko ya dunia yalivyo hivi sasa.

“Ilikuwa ni wiki ngumu ila wanahabari wataweza kuongeza kiwango cha uwandishi wao, husuasani katika kuandika habari huku wakiingiza na takwimu ndani yake”alisema Nuzulack.

Vilevile Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha waandishi wa habari za Mazingira Tanzania (JET), John Chikomo alisema mafunzo ya nishati jadidifu yamewashirikisha waandishi wa habari 20 kutoka mikoa yote ikiwemo ni pamoja na visiwa vya  Zanzibar, huku akiwataka kuhakikisha wanakuwa waandishi bora katika masuala ya nishati nchini.

“Wataweza kuripoti habari zinazohusu sekta ya nishati jadidifu kwa kina, pamoja na kusaidia na kuhamasisha jamii jinsi ya kutumia nishati jadidifu kwa maendeleo yao”alisema.

Hata hivyo   Makamu Mwenyekiti wa Tanzania Renewable Association Prosper R. Magali, aliwataka waandishi wa habari kupaza sauti zao ili kuwepo kwa sera na kanuni zinazohusiana na masuala ya nishati jadidifu moja kwa moja.

Alisema ili serikali kuweza kuwa na nishati mbadala ya kutosha nchini, lazima kuekeza fedha za kutosha katika miradi hiyo ya nishati njini.

Kwa upande wao waandishi wa habari wa masuala ya nishati jadidifu Tanzania, wamesema mategemeo yao ni kuwa waandishi nguli nchini katika masuala ya nishati mbadala.

 Waandishi wa habari za mazingira na nishati jadidifu wapo katika mafunzo ya miezi sita yatakayowasaidia kujua na kufahamu vyema faida za nishati hio na kutoa elimu kw aumma kupitia kalamu zao na  ya  yameandaliwa na Taasisi ya Nukta Afrika Tanzania na Chama cha Waandishi wa habari za Mazingira Tanzania (JET) kwa kushirikina na HIVOS.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...