Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa
Uwekezaji wa Norway (Norfund), Bw. Tellef Thorleifsson akiongea na
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof.
Palamagamba John Kabudi (Mb) wakati alipomtembelea ofisini kwake na
kufanya nae mazungumzo leo jijini Dar es Salaam
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa
Mfuko wa Uwekezaji wa Norway (Norfund), Bw. Erik Sandersen akiongea na
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof.
Palamagamba John Kabudi (Mb) (hayupo pichani) wakati ujumbe huo
ulipomtembelea ofisini kwake na kufanya nae mazungumzo leo jijini Dar es
Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)
akiongea na Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Uwekezaji wa Norway (Norfund), Bw.
Tellef Thorleifsson katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam
Balozi wa Norway nchini, Mhe.
Baalozi, Ms. Elisabeth Jacobsen akifafanua jambo mbele ya Waziri wa
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John
Kabudi (Mb) pamoja na Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Uwekezaji wa Norway
(Norfund), Bw. Tellef Thorleifsson
………………………………………………………………………………………………………….
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)
amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Uwekezaji
wa Norway kwa nchi zinazoendelea (Norwegian Investment Fund for
Developing Countries – Norfund), Bw. Tellef Thorleifsson.
Mazungumzo hayo yamefanyika leo
katika ofisi ndogo za wizara Jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo
mengine, Mhe. Waziri Prof. Kabudi pamoja na Bw. Thorleifsson wamejadili
masuala yanayohusu fursa za uwekezaji na biashara kati ya Tanzania na
Norway.
“Kwa kweli sisi tunafurahishwa na
mradi wa Africado ambao umewekezwa katika Wilaya ya Siha mkoani
Kilimanjaro kwani umekuwa ukizalisha maparachichi yanayopelekwa nchi
mbalimbali za Ulaya kama vile Uholanzi, Uingereza, Ufaransa, Hispania,
Ureno, na Mashariki ya Kati, na kuisaidia serikali kukuza pato lake la
taifa,” Amesema Prof. Kabudi na kuongeza kuwa mradi huo umetoa fursa za
ajira takribani 600 kwa wananchi wa Tanzania.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa
Mfuko wa Uwekezaji wa Norfund, Bw. Thorleifsson amesema kuwa lengo la
mkfuko huo ni kuwekeza katika miradi mbalimbali ndani ya nchi za Kusini
mwa Jangwa la Sahara ili kuzisaidia nchi hizo kukuza uchumi wake.
“Lengo letu ni kuwekeza katika
nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara ambapo hadi kufika mwishoni mwa 2018
tayari mfuko ulikuwa umewekeza nchini Tanzania kiasi cha Dola za
Marekani milioni 160 katika miradi mbalimbali katika sekta za nishati,
fedha, chakula na kilimo. Uwekezaji huo umeifanya Tanzania kuwa nchi ya
nne katika nchi zinazonufaika na miradi ya Norfund,” amesema Bw.
Thorleifsson
Norfund ni taasisi iliyo chini ya
Serikali ya Norway yenye jukumu la kuwekeza mitaji na utaalamu katika
uanzishwaji wa miradi mbalimbali endelevu kwenye nchi zinazoendelea kwa
lengo la kuchangia maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Ziara imetoa fursa
kwa pande zote mbili kuweza kujadili namna bora ya kuboresha maeneo ya
vipaumbele katika sekta ya uwekezaji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...