Serikali ya Kenya itatoa viburudisho kwa watu 30,000 wa kwanza kufika katika mazishi ya rais wa zamani wa Kenya Daniel arap Moi siku ya Jumatano.

Mratibu wa jimbo la Rift Valley Regional George Natembeya amesema kuwa kutakuwa na viti, soda, maziwa na mikate pamoja na maji kwa watu 30,000 wa kwanza kufika kwenye mazishi na pia watakalishwa kwenye hema.

Bwana Natembeya amesema kuwa waombolezaji waliosalia watakaribishwa tu ndani ya eneo la makazi, lakini hawatapata mahala pa kukaa.

Amesema pia kwamba vitafunio kwa wale watakaohudhuria mazishi wa kwanza vitatolewa: "atakayefika kwanza ndiye atakayepewa wa kwanza ", amesema Bwana Matembeya huku akiwataka waombolezaji kufika mapema kilioni

Usafiri utatolewa kuanzia mji wa Nakuru hadi katika makazi ya Moi ya Kabarak yapata kilomota 20 (sawa na maili 12.4) kutoka Nakuru mjini.

Baadhi ya wakenya kwenye mitandao ya kijamii wamekosoa vigezo kauli hiyo ya serikali ya kutolewa kwa viburudisho vya bure kwa waombolezaji.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...