Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa
Mataifa linaloshughulikia Uhamaji (IOM), kanda ya Kusini mwa Afrika Bw.
Charles Kwenin akiongea na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge leo
katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge
akiwaelezea jambo Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa
linaloshughulikia Uhamaji (IOM), kanda ya Kusini mwa Afrika Bw. Charles
Kwenin akiongea pamoja na Mwakilishi wa IOM hapa nchini Dkt. Qasim Sufi
leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge
(watatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa (IOM), Bw.
Charles Kwenin, Mwakilishi wa IOM nchini Dkt. Qasim Sufi pamoja na Afisa
Uhusiano na Sera wa IOM, Bi. Naomi Shiferaw. Wengine kulia mwa Katibu
MKuu ni watumishi wa Wizara, Bw. Hangi Mgaka na Gloria Ngaiza.
…………………………………………
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge,
amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa
Mataifa linaloshughulikia Uhamaji (IOM), kanda ya Kusini mwa Afrika Bw.
Charles Kwenin katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.
Pamoja na mambo mengine,
mazungumzo hayo yalijadili mambo mbalimbali ikiwemo maandalizi ya
Majadiliano kuhusu Uhamaji katika kanda ya Kusini mwa Afrika
yanayotarajia kufanyika chini ya uenyekiti wa Tanzania kama Mwenyekiti
wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC).
Majadiliano hayo yanatarajiwa
kufanyika kabla ya mwezi Agosti, mwaka 2020 hapa nchini yakiwa na
dhamira ya kujadili usimamizi wa masuala ya uhamiaji ili kuwezesha
uundwaji wa sera zenye uwiano miongoni mwa nchi wanachama wa SADC.
Aidha, Balozi Ibuge amewahakikishia wajumbe wa IOM, utayari wa Tanzania kuwa nchi mwenyeji wa Majadiliano hayo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...