

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally amewasili Mkoani Mtwara kwa ziara ya siku tatu.
Dkt. Bashiru amewasili asubuhi ya leo tarehe 21 Februari, 2020 uwanja wa ndege wa Mtwara mjini na kupokelewa na mamia ya wanachama, wapenzi na mashabiki wa CCM.
Katibu Mkuu atatembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika wilaya za Mtwara Vijijini na Masasi na kuzindua mashina ya wakereketwa wa CCM ikiwa ni muendelezo wa utekelezaji wa maagizo ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa kuendelea kujenga na kuimarisha Chama katika ngazi za mashina pamoja na kukagua miradi ya maendeleo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...