Jaji   Kiongozi   wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi ( wa kwanza kulia) akizungumza leo na ujumbe wa Benki ya Dunia (WB)  kuhusu mafanikio yaliyopatikana katika ripoti ya utafiti juu ya usikilizaji na umalizaji  wa mashauri ya jinai kwa wakati. Wa pili kulia ni Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Sharmillah Sirwatt na wengine ni baadhi ya viongozi wa Mahakama ya Tanzania.

Aidha   Jaji Kiongozi   aliueleza ujumbe huo kuhusu mabadiliko ya sheria mbalimbali yalivyowezesha usikilizaji wa mashauri ya jinai kwa haraka. Ujumbe huo uko nchini kwa ziara ya kikazi.
Ujumbe wa Benki ya Dunia (WB) na baadhi ya viongozi wa Mahakama ya Tanzania wakimsikiliza Jaji Kiongozi (ambaye hayupo pichani).
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi ( wa kwanza kulia) akifafanua jambo  leo kwa ujumbe wa Benki ya Dunia (WB)  kuhusu mafanikio yaliyopatikana katika ripoti ya utafiti juu ya usikilizaji na umalizaji  wa mashauri ya jinai kwa wakati. Wa pili kulia ni Msajili wa Mahakama  Kuu ya Tanzania, Mhe. Sharmillah Sirwatt na wengine ni baadhi ya viongozi wa Mahakama ya Tanzania.
Mtaalamu wa Benki ya Dunia (WB), Bw. Waleed Malik (wa pili kushoto) akifafanua jambo wakati wa mazungumzo hayo.
Mtaalamu wa Benki ya Dunia (WB), Bi. Debohar  Isser (wa kwanza kushoto) akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo hayo, ( wa tatu kushoto)  ni Bi. Clara Maghani na  (wa nne   kushoto)  ni Bw. Denis Biseko (wote ni wataalamu kutoka WB). (Picha na Magreth Kinabo – Mahakama ya Tanzania)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...