Woinde Shizza,Michuzi Tv Arusha
Jumuiya  ya Afrika  mashariki imeshauriwa  kubuni vyanzo  vya mapato  vitakavyoiwezesha  kujiendesha  bila  kutegemea  Michango inayotolewa  na  nchi  wanachama  na pia  wafadhili
Mjadala  huo  uliibuka  wakati  wabunge wakichanganua ripoti ya  ukaguzi  wa  mahesabu za jumuiya a hiyo baada  ya  mbunge  kutoka Uganda suzan Nakawuki kulieleza Bunge  kuwa kuna haja ya hatua  za kisheria  kuanza  kuchukuliwa  kwa  idara ama watendaji  wasiotimiza wajibu wao na kusababisha  baadhi ya matatizo  kujirudia
Hata hivyo  hoja hiyo pamoja  na  hoja hiyo   kuwa  na  lengo  ka  kufanikisha  mipango na  kufikia  malengo , baadhi  ya  wabunge akiwemo pamela maasai kutoka Tanzania  wamesema kutumia sheria  ama  katika  suala  hilo hakutakuwa  na tija  kwani kimsingi  masuala  mengi  ya jumuiya  yanaendeshwa kwa  mfumo wa majadiliano ,kushauriana  na  kuvumiliana
Aidha  pia mbunge huyo  akatoa mapendekezo  kwa jumuiya  kuangalia upya  namna ya kupata fedha  za  kujiendesha  bila  kutegemea michango  ya nchi  wanachama  kwa asilimia kubwa  na pia ile inayotolewa  na  wafadhili .
Mariamu  Ussi   ni  Mbunge  wa bunge  hilo kutoka  Tanzania  anabainisha baadhi ya  athari zinazojitokeza   kutokana  na  ukosefu  wa  fedha  za  kutosha ikiwemo  ya jumuiya  kushindwa  kukidhi mahitaji muhimu  yakiwemo ya  wafanyakazi.
Tatizo  la  ukosefu wa fedha  katika  Jumiya ya  Afrika  mashariki  limekuwa  likijitokeza mara   kwa mara na kulalamikiwa  na wabunge  wa bunge  hilo na pia licha  ya  kuwa  limekuwa likishughulikiwa   baadhi  ya wabunge  wanasema kasi  yake ni  ndogo .
Jumuiya  hiyo  ya afrika amashariki inayoundwa  na  nchi  sita za Tanania Kenya ,Uganda , Rwanda ,Burundi  na sudani kusini ikikadiriwa  kuwa na watu  wapatao  milioni 173 kwa  asilimia  kubwa inaendeshwa  kwa  michango inayotolewa  na  nchi  wanachama na pia  inayotolewa  na  wafadhili .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...