Wizara ya afya ya Misri imetangaza kisa cha kwanza kilichothibitishwa cha mgonjwa wa virusi vya Corona kinachokuwa cha kwanza pia barani Afrika.

Taarifa iliyotolewa na wizara hiyo imesema mgonjwa aliyebainika siyo raia wa Misri lakini pia haikufafanua uraia wa mtu huyo.

Maafisa wa Misri walifanikiwa kuthibitisha kisa hicho kupitia mpango ulioanzishwa na serikali wa kuwafuatilia abiria waliowasili kutoka nchini ambazo virusi vya Corona tayari vimesambaa.

Msemaji wa wizara ya afya ya Misri, Khaled Megahed, amesema serikali imechukua hatua za tahadhari na inafuatilia kwa karibu afya ya mgonjwa huyo ambayo imeripotiwa kuwa imara.

Mamlaka za Misri pia zimeliarifu shirika la afya duniani WHO kuhusiana na kisa hicho na tangu wakati huo mgonjwa huyo amewekwa karantini katika hospitali maalum ya umma. 

Raia walirejeshwa kutoka China wamewekwa Karantini.

Mapema mwezi huu Misri ilifuta safari zote za ndege za shirika la ndege ya taifa kwenda China. Na hatua hiyo itaendelea hadi mwishoni mwa mwezi huu.

Raia 301 na moja wa Misri waliondolewa kutoka mji wa Wuhan, kitovu cha mripuko huo wa virusi nchini China na tangu walipowasili wamewekwa karantini ya siku 14.

Mahusiano ya karibu na China na mifumo dhaifu ya afya ni masuala yanayozua wasiwasi kuhusu uwezo wa nchi za Afrika wa kukabilina na mripuko wa virusi vya Corona vinavyyowauwa maelfu ya watu nchini China.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...