Wizara ya afya ya Misri imetangaza kisa cha kwanza kilichothibitishwa
cha mgonjwa wa virusi vya Corona kinachokuwa cha kwanza pia barani
Afrika.
Taarifa iliyotolewa na wizara hiyo imesema mgonjwa aliyebainika siyo raia wa Misri lakini pia haikufafanua uraia wa mtu huyo.
Maafisa
wa Misri walifanikiwa kuthibitisha kisa hicho kupitia mpango
ulioanzishwa na serikali wa kuwafuatilia abiria waliowasili kutoka
nchini ambazo virusi vya Corona tayari vimesambaa.
Msemaji wa
wizara ya afya ya Misri, Khaled Megahed, amesema serikali imechukua
hatua za tahadhari na inafuatilia kwa karibu afya ya mgonjwa huyo ambayo
imeripotiwa kuwa imara.
Mamlaka za Misri pia zimeliarifu shirika
la afya duniani WHO kuhusiana na kisa hicho na tangu wakati huo mgonjwa
huyo amewekwa karantini katika hospitali maalum ya umma.
Raia walirejeshwa kutoka China wamewekwa Karantini.
Mapema mwezi huu Misri ilifuta safari zote za ndege za shirika la
ndege ya taifa kwenda China. Na hatua hiyo itaendelea hadi mwishoni mwa
mwezi huu.
Raia 301 na moja wa Misri waliondolewa kutoka mji wa
Wuhan, kitovu cha mripuko huo wa virusi nchini China na tangu
walipowasili wamewekwa karantini ya siku 14.
Mahusiano ya karibu
na China na mifumo dhaifu ya afya ni masuala yanayozua wasiwasi kuhusu
uwezo wa nchi za Afrika wa kukabilina na mripuko wa virusi vya Corona
vinavyyowauwa maelfu ya watu nchini China.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...