Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) kimetoa adhabu mbalimbali wa wachezajiz timu na viongozi wa mpira baada ya kukiuka kanuni za ligi kuu Tanzania bara.

Maamuzi hayo yametolewa leo baada ya kikao chake cha Februari 10, 2020 ambacho kilipitia mwenendo na matukio mbalimbali ya Ligi na kufanya uamuzi yafuatayo.;

Ligi Kuu ya Vodacom:

Mechi namba 178: Simba SC 2 v Coastal Union
FC 0

Kocha wa Simba Steven Vanden Broeck amepewa Onyo Kali kwa kosa la kugoma kuwafungulia mlango mwamuzi na Kamishina wa mchezo wakati wa ukaguzi wa timu katika mechi hiyo iliyochezwa Februari 01,2020 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Adhabu hiyo imetolewa kwa mujibu wa Kanuni namba 41(13) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Makocha.

Mechi namba 188: Simba SC 2 VS Polisi Tanzania FC 1

Klabu ya Polisi Tanzania imepigwa Faini ya kiasi cha Tsh.1,500,000/=(Milioni Moja na Laki Tano) kwa kosa la kutumia mlango usio rasmi wa kuingia Uwanjani katika mechi iliyochezwa Februari 04,2020 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.Adhabu hii imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(14) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo
Vile vile katika mchezo huo Kocha Mkuu wa Klabu ya Simba Sc Steven VandenBroeck ametozwa Faini ya kiasi cha Tsh.500,000/=(Laki Tano) kwa kosa la kugoma kuongea na waandishi wa habari mara baada ya mchezo kumalizika.Adhabu hii ni kwa kuzingatia Kanuni namba 41(12) kuhusu Udhibiti wa Makocha.

Mechi namba 189:Azam Fc 1 vs Tanzania Prisons Fc 1

Mchezaji wa Klabu ya Azam Fc Agrrey Moris amepigwa Faini ya kiasi cha Tsh.200,000/=(Laki Mbili) kwa kosa la kugoma kuongea na waandishi wa habari mara baada ya mchezo kumalizika katika mechi iliyochezwa Februari 05,2020 katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.Adhabu hii imetolewa kwa mujibu wa Kanuni namba 38(18) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Wachezaji.

Mechi namba 190:Yanga Sc 2 vs Lipuli Fc 1

Mwamuzi Abubakar Mturo amefungiwa miezi mitatu(3) kwa kosa la kushindwa kumudu mchezo katika mechi iliyochezwa Februari 05,2020 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni namba 39(1) ya Ligi Kuu Kuhusu Udhibiti wa Waamuzi.

Vile vile katika mchezo huo mwamuzi msaidizi namba mbili Joseph Pombe amefungiwa miezi mitatu(3) kwa kosa la kushindwa kumudu mchezo. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni namba 39(1) ya Ligi Kuu Kuhusu Udhibiti wa Waamuzi.

Mechi namba 191:Simba SC (0) vs JKT Tanzania (1)

Mwamuzi msaidizi namba mbili Kassim Mpanga Amefungiwa miezi mitatu(3) kwa kosa la kushindwa kutafsiri sheria za mpira wa miguu katika mechi iliyochezwa Februari 07,2020 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni namba 39(1) ya Ligi Kuu Kuhusu Udhibiti wa Waamuzi.


Ligi Daraja la Pili:

Mechi namba 19C : DTB Fc 1 vs Tukuyu Stars 0

Klabu ya DTB iliomba marejeo kuhusiana na mchezo huo na Kamati imepitia na kukubaliana na utetezi wao hivyo matokeo yatabaki kama yalivyokuwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...