Kamishna Jenerali mpya wa Magereza, Suleiman Mzee akipokea salaam ya
heshima toka katika Gwaride Maalum lililoandaliwa na Maofisa na askari
wa Jeshi la Magereza(hawapo pichani) kwa ajili yake kwa heshima leo
katika Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya Magereza, Jijini Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali mpya wa Magereza, Suleiman Mzee akikagua Gwaride
Maalum lililoandaliwa na Maofisa na askari wa Jeshi la Magereza kwa
ajili yake kwa heshima kama inavyoonekana katika picha.
Kamishna Jenerali mpya wa Magereza, Suleiman Mzee akisalimiana na
aliyekuwa Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike(sasa Balozi
mteule) alipowasili Makao Makuu ya Jeshi hilo baada ya kuapishwa rasmi
kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza leo, Ikulu Jijini Dar es
Salaam Februari 3, 2020. Kulia ni Kamishna wa Utawala na Rasilimali Watu
wa Jeshi hilo, Uwesu Ngarama.
Kamishna Jenerali mpya wa Magereza, Suleiman Mzee akifanya mahojiano
maalum na wanahabari baada ya kuwasili katika Ofisi ndogo za Makao Makuu
ya Jeshi la Magereza jijini Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali mpya wa Magereza, Suleiman Mzee akiongea na Maafisa,
Askari na Watumishi raia wa Jeshi la Magereza baada ya kutoka kuapishwa
kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, Ikulu Jijini Dar es Salaam
Februari 3, 2020.
Baadhi ya Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza wakimsikiliza Kamishna Jenerali mpya wa Magereza, Suleiman Mzee mara baada ya kutoka kuapishwa kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza leo, Ikulu Jijini Dar es Salaam Februari 3, 2020(Picha zote na Jeshi la Magereza).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...