Mitandao ya kijamii   imeongeza wigo katika ajira kwa vijana kufanya ubunifu mbalimbali ikiwemo uuzaji wa bidhaa kwa kutumia mitandao hiyo.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Melisa Lilian Ringo wakati akizindua App kwa ajili ya Keki iliyofanyika leo, jijini Dar es Salaam.

Ringo amesema kuwa watu wanaohitaji Keki watakwenda kwenye mtandao na kufungua 'Melisa Cake'  na kuchagua aina mbalimbali za Keki.Amesema mteja akiingia katika App hiyo atachagua Keki aitakayo baada ya hapo  Kampuni itapeleka keki moja kwa moja kwa mteja .

Ringo amesema wanatengeneza keki za matukio mbalimbali na  bei zake kila mtanzania  anaweza kumudu.

Aidha amesema kuwa licha ya kutengeneza keki wanauza vifaa vya kutengeneza Keki pamoja na kuwapo kwa madarasa ya kutengeneza Keki."Tanzania ya Viwanda tuitumie kwa kutengeneza vitu mbalimbali vinavyotuzunguka kutokana na mahitaji ya kiwanda, sio lazima uwe na mtambo mkubwa"amesema Ringo.

Hata hivyo amesema kuwa bidhaa ya Keki ipo lakini sasa watakwenda kisasa kwa kutumia mitandao kuzungumza gharama ya kutoka sehemu Mmoja kwenda nyingine.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Melisa Lilian Ringo akionesha Aina ya Keki waliotengeneza kwa ajili ya uzinduzi katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Melisa Lilian Ringo akikata keki mara baada ya uzinduzi wa App ya Melisa Cake iliyofanyika jijini Dar es Salaam
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Melisa  Lilian Ringo akizungumza na waandishi habari kuhusiana na uzinduzi wa App kwa ajili ya uuzaji wa Keki katika mtandao kwa kufungua Melisa Keki,jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...