Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa (kushoto), akitembelea mabanda ya maonyesho ya wadau wa sekta ya madini wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini uliomalizika juzi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. NBC ilidhamini mkutano huo. Anayemuongoza katikati ni Waziri wa Madini, Doto Biteko. 
Kamishna wa Tume ya Madini, Prof. Abdulkarim Mruma, akishikana mikono na Meneja Mahusiano wa Taasisi za Umma wa Benki ya NBC, Azza Mnzava (wa pili kushoto), mara baada ya kamishna huyo kutembelea banda la NBC wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini uliomalizika juzi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. NBC ilidhamini mkutano huo. Wengine kushoto ni Wakala wa Mauzo katika Kitengo cha Hazina na Masoko ya Fedha za Kigeni, Emmanuel Gasirabo (kushoto), na Meneja Mahusiano Kitengo cha Wateja Rejerejea Maalumu, Daniel Kaila.


Wakala wa Mauzo katika Kitengo cha Hazina na Masoko ya Fedha za Kigeni wa Benki ya NBC, Emmanuel Charles Gasirabo akihojiwa na vyombo vya habari wakati wa mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini uliomalizika mwishoni mwa wiki iliyopita katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. NBC ilidhamini mkutano huo.
Meneja Masoko wa NBC, Alina Maria Kimaryo, akisalimiana Makamu wa Rais wa Kampuni ya Geita Gold Mine, Simon Shayo baada ya kutembelea banda la NBC wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini uliomalizika juzi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. NBC ilidhamini mkutano huo. Kulia ni Ofisa Mahusiano wa NBC kitengo cha Wateja Maalumu, Daniel Kaila. 
Meneja Masoko wa Benki ya NBC, Alina Maria Kimaryo (kulia), akizungumza na Makamu wa Rais wa Kampuni ya Geita Gold Mine, Simon Shayo baada ya kutembelea banda la NBC wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini uliomalizika juzi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. NBC ilidhamini mkutano. Wanaoangalia kutoka kushoto ni Meneja Mahusiano wa Taasisi za Umma wa NBC, Azza Mnzava na Wakala wa Mauzo katika Kitengo cha Hazina na Masoko ya Fedha za Kigeni, Emannuel Gasirabo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...