Benki ya NMB imesema itahakikisha inaendelea na kuunga mkono juhudi za maendeleo ya Serikali ya awamu ya tano ili kuifikia malengo yaliyokusudiwa ya kuwahudumia wananchi .

Kauli hiyo ilitolewa Mkuu wa idara ya huduma za Serikali wa benki ya NMB, Vicky Bishubo wakati alipokuwa akiwasilisha taarifa ya benki hiyo kwenye mkutano wa utoaji taarifa ya mafanikio ya miaka minne ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) uliofanyika Jijini Dodoma.

“Benki ya NMB ni mali ya wananchi na Serikali hivyo tunafurahi tunapoona kila upande unaendelea kuiunga mkono katika mafanikio yaliyopatikana hivyo tunawaomba mwendelee kutuunga mkono kwa kufungua akaunti na kuweka fedha kwetu”alisema.

Bishubo alisema Benki ya NMB itahakikisha inaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ili kufikia malengo ya kuwahudumia wananchi wake katika maeneo mbalimbali nchini.

Alisema benki hiyo inaendelea kufungua matawi na kuweka mashine za ATM katika maneo mbalimbali ili kuhakikisha wananchi wanafikiwa na huduma za kibenki karibu na maaneo yao.

Alibainisha kuwa uwepo wa benki hiyo katika kila Wilaya hapa nchini imesaidia pia kurahisisha maendeleo ya wananchi kwa kupata huduma za kifedha karibu kwenye maeneo yao. Aliongeza pia benki hiyo imeweka mawakala wengi hapa nchini kwa lengo la kuwasogezea wananchi huduma za kifedha katika maeneo yao.

Aidha alisema benki hiyo imekuwa ni sehemu ya mafanikio ya Ofisi ya Tamisemi kutokana na kufanyakazi kwa karibu na Halmashauri zote hapa Nchini.

Kwa upande Waziri Selemani Jafo alitaja baadhi ya mafanikio ya Ofisi hiyo kuwa ni ujenzi wa vituo vya afya 97 zimejengwa na vingine kukarabatiwa na Serikali katika kipindi hicho cha miaka minne ya mafanikio

Jafo alitaja mafanikio mengine kwenye sekta ya elimu kuwa ni ongezeko la ufaulu wa wanafunzi, ujenzi wa vyumba vya madarasa na ukarabati wa majengo ya shule kongwe hapa nchini.

Hata hivyo aliwashukuru benki ya nmb kwa kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kutoa misaada mbalimbali kwenye sekta ya afya na elimu hapa nchini.#NMBKaribuYako.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI)- Mhe. Selemani Jafo akimkabidhi taarifa ya mafanikio ya miaka minne ya wizara hiyo  Mkuu wa Idara ya Huduma za Serikali wa NMB - Vicky Bishubo mara baada ya kuwasilishwa mwisho wa wiki,  Jijini Dodoma. Kushoto ni Naibu Waziri Wizara hiyo Mhe. Mwita Waitara.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) - Mhe. Selemani Jafo akisalimiana na Mkuu wa Idara ya Huduma za Serikali wa Benki ya NMB - Vicky Bishubo walipokutana katika mkutano wa utoaji taarifa ya mafanikio ya  TAMISEMI .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...