Mgeni rasmi wa Tamasha hilo lililoandaliwa na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo alikuwa ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Selemani Jaffo akiambatana na Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu na Mbunge wa Viti Maalumu Pwani Zainabu Vullu.

Akizungumza na wananchi wa Kisarawe , Jaffo amewataka wananchi wa Kisarawe kulinda miundo mbinu ya maji kwani serikali imetumia gharama kubwa kuweza kufanikisha mradi huo mkubwa wa maji.

Amesema, kiasi cha Shillingi bilion 10.6 zimetumika katika kujengwa kwa mradi huo na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira DAWASA na kwa sasa wananchi wa Kisarawe wanapata maji safi kwa muda wote.

"Mradi huu wa maji umetumia fedha nyingi sana, na maji yanapatikana masaa 24 tuna tenki linalohifadhi lita Milion 6 na mahitaji ya Mji wa Kisarawe ni Lita milion 1.2 na tayari kuna akiba ya Lita Milion 4.8," amesema.

"Na kwakuwa tayari maji yapo ya kutosha, nawaagiza Dawasa wamepeleka maji kwenye maeneo ambayo huduma ya maji safi haijafika na kwakuwa nyinyi ni watendaji wazuri naamini hilo litafanikiwa,"

Aidha, Jaffo amesema huduma ya maji imechochea zaidi katika kuboresha huduma bora kwa wajasiriamali hususani wakina mama lishe ikiwapunguzia gharama za kununua maji kwa bei kubwa.

"maendeleo yanakuja kama kuna upatikanaji wa maji na nishati wakutosha, sasa maji Kisarawe yapo milango iko wazi kwa wawekezaji na pia wakina mama huu ndio muda wenu wa kutumia fursa"

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo amesema kuwa wameamua kuandaa tamasha la Kisarawe Mamalishe Festival katika kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo hufanyika machi 8 kila mwaka.

Amesema,asilimia 65 ya wanawake wa Kisarawe wanajishughulisha na shughuli ya mama lishe na lengo likiwa ni kuwakutanisha wakinamama hao ili wabadilishane mawazo.

"Tukiongelea katika sekta ya maji, Dawasa wamefanya kazi kubwa sana sasa hivi tuna mradi mkubwa wa maji na wananchi wanaendelea kuunganishwa tunaishukuru sana serikali ya awamu ya tano kwa kutuletea maji Kisarawe,"

Meneja wa Mahusiano Dawasa  Everlasting Lyaro ameeleza wanaendelea kuunganisha wateja wapya na muitikio umekuwa ni mkubwa sana toka mradi huo uanze kufanya kazi.

Na wamepokea maagizo ya Waziri Jaffo watayatekeleza ili wananchi wote wa Wilaya ya Kisarawe wapate maji safi na ya uhakika.

Wasanii mbalimbali waliweza kuhudhuria akiwamo Shilole, Aunt Ezekiel, Jackline Wolper, Meja Kunta, Sholo Mwamba na wengineo

  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Selemani Jaffo  akizungumza na wananchi wakati wa Tamasha la Kisarawe Mama Lishe Festival lililofanyika leo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na wasanii.
 Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo akizungumza na wananchi wakati wa Tamasha la Kisarawe Mama Lishe Festival lililofanyika leo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na wasanii.
 
 Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo akionesha zawadi ya vyombo kwa Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu na Mbunge wa Viti Maalumu Pwani Zainabu Vullu.watakaokabidhiwa washindi wa kupika  wakati wa Tamasha la Kisarawe Mama Lishe Festival lililofanyika leo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na wasanii.





 
 Wakina mama Lishe wakiwa wanaendelea na maandalizi ya chakula wakati wa Tamasha la Kisarawe Mama Lishe Festival lililofanyika leo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na wasanii.
Wakina mama Lishe wakiwa wanaendelea na maandalizi ya chakula wakati wa Tamasha la Kisarawe Mama Lishe Festival lililofanyika leo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na wasanii.
Picha ya pamoja ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Selemani Jaffo  Mbunge wa Viti Maalumu Pwani Zainabu Vullu, Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo na Meneja Uhusiano Dawasa Everlasting Lyaro na Meneja wa Mkoa wa Kihuduma Kisarawe Ernest Mbwambo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...