Akiwa ameketi chini kudondoa maharagwe, miguu ya Margaret Tindimutuma iliyofura ina maumivu.

Mama huyo anaugua aina ya ugonjwa wa matendee ambao ni nadra sana na umetaabisha sana familia yake.

"Kila wakati mimi huwa na mzio tangu nikiwa mdogo. Kwa hiyo miguu yangu ilipoanza kufura na kufanya kama majipu, nilichukulia ni jambo la kawaida," mama huyo mwenye umri wa miaka ya 80, anasema hivyo akiwa ameketi mkekani katikati ya uwanja wa nyumbani kwake.

"Lakini maumivu yaliendelea kuongezeka, nilikuwa ninahisi kuchomwa mwili mzima. Ngozi katikati ya vidole vya miguuni ilianza kupasuka na kufanya vidonda. Kisha vijana wangu wakaanza kuumwa. Na hapo ndipo nilipoanza kujiuliza kama pengine nimewarithisha ugonjwa huo."

Vijana wake wawili walifariki 2017, na mwaka uliotangulia baada ya kupata vidonda mguuni na baadaye kupata maambukizi ya ugonjwa huu. 
 
Chanzo: BBC Swahili

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...