Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) Mhe. Angellah Kairuki akihutubia wakati wa Mkutano wa mashauriano kati ya Serikali na Sekta binafsi ili kusikiliza changamoto za wawekezaji na wafanyabiashara na kuzipatia ufumbuzi uliofanyika katika Manispaa ya Shinyanga Februari 26, 2020.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Tellack akieleza kuhusu fursa za uwekezaji zilizopo katika mkoa wake wakati wa Mkutano wa mashauriano kati ya Serikali na Sekta binafsi ili kusikiliza changamoto za wawekezaji na wafanyabiashara na kuzipatia ufumbuzi uliofanyika katika Manispaa ya Shinyanga Februari 26, 2020.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni akisalimiana na Mhe.Steven Masele (Mb) wakati wa Mkutano huo.
Naibu Waziri Maliasili na Utalii Mhe. Constantine Kanyasu akijibu hoja wakati Mkutano wa mashauriano kati ya Serikali na Sekta binafsi ili kusikiliza changamoto za wawekezaji na wafanyabiashara na kuzipatia ufumbuzi uliofanyika katika Manispaa ya Shinyanga  mkoani Shinyanga.
Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega akijibu hoja za masuala ya wafugaji na wavuvi wakati wa mkutano huo.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angelina Mabula akijibu hoja za masuala ya wafugaji na wavuvi wakati wa mkutano huo.
Mmoja wa wachimbaji wadogo mkoa wa Shinyanga Bw. Ludaki Shaban akiwasilisha kero za ukosefu wa umeme katika maeneo ya uchimbaji wakati wa mkutano wa kusikiliza changamoto za wawekezaji na wafanyabiashara katika mkoa huo.
Mmoja wa wafanyabiashara mkoa wa Shinyanga Bw. Idsam Mapande akiwasilisha hoja zinazohusu kero za madereva pikipiki wakati wa mkutano huo.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza wakati wa mkutano huo
Baadhi ya washiriki wa Mkutano wa mashauriano kati ya Serikali na Sekta binafsi ili kusikiliza changamoto za wawekezaji na wafanyabiashara na kuzipatia ufumbuzi uliofanyika katika Manispaa ya Shinyanga wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Nchi Ofisi (Uwekezaji) Mhe. Angellah Kairuki (hayupo pichani) Februari 26, 2020.
(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)
…………………………………………………………………………………………………….
  1. MWANDISHI WETU
Zaidi ya wafanyabiashara na wawekezaji 560 mkoani Shinyanga wamekutana katika mkutano wa mashauriano baina ya Serikali na Sekta binafsi ili kusikilizwa na kupata ufumbuzi wa changamoto katika maeneo yao ya uwekezaji na biashara ili kuendelea kuwa na tija katika maendeleo yao na nchi kwa ujumla.
Mkutano huo ulililofanyika tarehe 26 Februari, 2020 ulioandaliwa na  Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkoa wa Shinyanga na  kufanyika  katika Ukumbi wa mikutano wa NSSF mkoani humo.
Mkutano ulijumuisha makundi yote ikiwemo, wakulima, wafugaji, wafanyabiashara wakubwa na wadogo, wachimba madini, wavuvi pamoja na wenye viwanda na  wawekezaji katika sekta mbalimbali.
Mkutano ulihudhuriwa na Mawaziri na Manaibu mawaziri kutoka Wizara nane ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Wizara ya Fedha na Mipango, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Mambo ya Ndani, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,Wizara ya Maliasili na Utalii na Wizara ya Madini.
Akizungumza wakati wa kufunga mkutano huo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Uwekezaji nchini Mhe.Angellah Kairuki alieleza namna Serikali ilivyoendelea na jitihada za kuhakikisha uboreshwaji wa mazingira ya uwekezaji nchini ikiwa ni pamoja na kutungwa kwa sheria mpya ya uwezeshaji biashara (Business Facilitation Acts)
Aidha sheria itasaidia kufanya mapitia ya sera na sheria stahiki kwa lengo la kuboresha mazingira ya uwekezaji na biashara nchini.
Aliongezea kuwa, uwepo wa mikutano hiyo inaongeza hamasa kwa wafanyabiashara na wawekezaji kueleza kero wanazokabiliana nazo pamoja na kupatiwa majibu ya papo kwa hapo na Mawaziri wa Sekta husika.
“Mikutano imeibua hoja muhimu zilizopatiwa ufumbuzi na mawaziri wa sekta mbalimbali  niwatoe shaka Serikali itaendelea kuwaunga mkono na ni vyema mkaendelea kufuata sheria na kanuni zilizopo katika kuwekeza kwenu,”.alisisitiza Waziri Kairuki.
Naye Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amewahakikishia wafugaji wa samaki kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira bora ya kuwawezesha wafugaji kufuga samaki na kueleza kuwa, mabwawa ya samaki yameongezaka kutokana na jitihada zilizopo na kueleza namna Serikali inavyoendelea kudhiti uvuvi haramu baharini na maziwa.
Sambamba na hili Naibu Waziri alieleza kuwa  jitihada za ujenzi wa viwanda vikubwa vya kuchakata mazao yatokanayo na mifugo nchini zinaendelea hivyo wananchi hawana budi kuwa na matumaini makubwa na Serikali yao.
Aidha Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashantu Kijaji aliwahaikishia wajumbe wa mkutano huo namna wizara yake ilivyojipanga kuondoa changamoto za gharama kubwa za mikopo katika benki pamoja na suala la utitiri wa kodi baada ya kulalamikiwa na wafanyabiashala hao.
“Nimewafurahia wana Shinyanga kwa uwazi wenu wa kujieleza vizuri, niwahakikishie kuwa,mwisho wa malalaiko yenu haupo mbali tutahakikisha sekta ya fedha inatatua kero zenu na kushughulikia upatikanaji wa mikopo na kwa gharama zinazoeleweka,”alieleza Dkt. Kijaji
Serikali imefanya jitihada kubwa kuhakikisha Taasisi zetu za mikopo zinashusha gharama za mikopo (riba) kwa ajili ya shughuli za kijamii zinazowahusu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...