Waathiriwa wa kirusi cha corona nchini Kenya wamefikia watu saba baada ya watu wengine watatu kuthibitishwa kuambukizwa kirusi hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano, Waziri wa Afya wa Kenya, Mutahi Kagwe amesema kuwa, watu wote hao saba wametoka nje ya Kenya. Wawili kati ya wagonjwa hao watatu wa karibuni kabisa wametokea Madrid Uhispania kupitia Dubai na mgonjwa wa tatu ni raia wa Burundi aliyewasili katika Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi akitokea Dubai pia.
Huku hayo yakiripotiwa, Wizara ya Afya ya Afrika Kusini imetangaza kuongezeka idadi ya waathiriwa wa kirusi cha corona nchini humo na kufikia watu 85 ikiwa ni ongezeko la watu 34 ikilinganishwa na taarifa ya kabla yake.
Kabla ya hapo Wizara ya Afya ya Afrika Kusini ilikuwa imetangaza kuwa watu 51 wameambukizwa kirusi cha corona nchini humo.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano, Waziri wa Afya wa Kenya, Mutahi Kagwe amesema kuwa, watu wote hao saba wametoka nje ya Kenya. Wawili kati ya wagonjwa hao watatu wa karibuni kabisa wametokea Madrid Uhispania kupitia Dubai na mgonjwa wa tatu ni raia wa Burundi aliyewasili katika Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi akitokea Dubai pia.
Huku hayo yakiripotiwa, Wizara ya Afya ya Afrika Kusini imetangaza kuongezeka idadi ya waathiriwa wa kirusi cha corona nchini humo na kufikia watu 85 ikiwa ni ongezeko la watu 34 ikilinganishwa na taarifa ya kabla yake.
Kabla ya hapo Wizara ya Afya ya Afrika Kusini ilikuwa imetangaza kuwa watu 51 wameambukizwa kirusi cha corona nchini humo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...