Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
SERIKALI
ya China kupitia ubalozi wake nchini utafadhili vifaa vya kupambana na
virusi vya Corona (Covid 19) ikiwemo kutoa vifaa vya kupima virusi hivyo
pamoja na kutoa vitakasa mikono (sanitizers) ambazo zitatolewa kwa
wananchi wa hali ya chini ikiwa ni sehemu ya mapambano dhidi ya virusi
hivyo vinavyosambaa katika maeneo mbalimbali duniani.
Akizungumza
leo jijini Dar es Salaam mara baada ya kutembelea kiwanda cha
uzalishaji bidhaa binafsi ikiwemo vitakasa mikono (saniters) cha
Traidea, Mkuu wa Mkoa huo Paul Makonda amesema kuwa tangu shirika la
afya duniani (WHO) litangaze kuzuka kwa ugonjwa huo Mkoa huo wenye
wakazi milioni 6 ni watu watatu pekee wamegundulika kuwa na virusi
hivyo.
"Nimetembelea
kiwanda hiki na nimewaomba waongeze kasi ya uzalishaji wa vitakasa
mikono licha ya kuwa na changamoto za rasilimali za kutosha za
kuwawezesha katika uharakishaji wa rasilimali hizo ili bidhaa ziwe za
kutosha kutokana na mahitaji ya jamii" ameeleza.
Amesema kuwa taarifa zote kuhusiana na janga hilo la kidunia zinatolewa na Wizara ya Afya ambayo ina mamlaka;"
Sio kila anayepelekwa hospitali ana Corona, kuzuka kwa Corona
hakujasimamisha magonjwa mengine hivyo tusiwe wasemaji wa mambo
tusiyoyajua, mitandao ya kijamii itumike vizuri" ameeleza Rc Makonda.
Pia
Makonda ameiomba Wizara ya Fedha kupunguza Kodi za rasilimali za
vitakasa mikono kwa kuwa kupanda kwa bei kwa rasilimali hizo na kufungwa
kwa viwanda kwa baadhi ya nchi kumepelekea kupanda kwa bei ya bidhaa
hizo sokoni.
Vilevile
amewataka wananchi kufuata taratibu za afya zinazoelekezwa kila siku na
hiyo ni pamoja na kutowanyanyapaa au kuwaficha waliopatwa na virusi
hivyo, kutokusanyika sehemu ambazo sio muhimu ili kujikinga zaidi na
virusi hivyo.
Kwa upande
wake Mkurugenzi wa kiwanda hicho Payal Kotecha amesema kuwa kiwanda
hicho kimewekeza ndani ya miaka minne katika harakati za kuunga mkono
jitihada za Serikali ya awamu ya tano katika ujenzi wa viwanda nchini na
kimekuwa kikitoa ajira kwa wazawa.
Amesema
kuwa kupanda bei kwa vitakasa mikono kumetokana na kukosekana na viungo
na malighafi na wameiomba Serikali kusimamia hilo ili malighafi hizo
ziingie nchini kwa uharaka zaidi.
Payal
amewashauri wananchi kufuata kanuni na taratibu zinazotolewa na Wizara
ya Afya kila siku na kueleza kuwa ushirikiano utafanikisha kutokomeza
kuenea kwa virusi hivyo ambavyo vimesambaa duniani kote.
.Mkurugenzi wa kiwanda cha uzalishaji bidhaa binafsi ikiwemo vitakasa
mikono Payal Kotecha (kushoto) akitoa maelekezo ya kiwanda hicho kwa
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda (katikati) kulia ni
Mkurugenzi wa uendeshaji wa kiwanda hicho Kishan Gokani, leo jijini Dar
es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda (katikati) akizungumza mara
baada ya kutembelea kiwanda cha kutengeneza bidhaa binafsi ikiwemo
vitakasa mikono cha Tradea ambapo amesema kuwa wananchi wafuate taratibu
za afya zinazotolewa kila siku pamoja na kutokuwa wasemaji wa mambo
wasiyoyafahamu, leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa kiwanda cha uzalishaji wa bidhaa binafsi
ikiwemo vitakasa mikono Payal Kotecha (kushoto) akizungumza na waandishi
wa habari mara baada ya mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda
kutembelea kiwanda hicho ambapo ameiomba Serikali kusimamia malighafi
ili ziingie nchini, leo jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...