Idadi ya wagonjwa wa virusi vya corona (Covid-19) katika nchi za Afrika Mashariki za Uganda na Rwanda imepaa kwa kasi huku nchi hizo zikipambana kuzuia maambukizi zaidi.
Nchini Uganda jana usiku wametangaza wagonjwa wapya nane na kufikisha idadi ya wagonjwa wa Covid-19 kufikia tisa.
Wagonjwa hao wapya wanane wote ni raia wa Uganda ambao wamerejea nchini humo kutokea Dubai baina ya tarehe 20 na 22 mwezi huu.
Waziri wa Afya wa Uganda, Jane Ruth Aceng amewaambia wanahabari kuwa kufikia sasa nchi hiyo imebaini wasafiri 2,661 wakiwemo raia wa nchi hiyo ambao wanaweza kuwa na hatari ya kusambaza maambukizi na watu wote hao wapo chini ya uangalizi maaalumu.
Nchini Uganda jana usiku wametangaza wagonjwa wapya nane na kufikisha idadi ya wagonjwa wa Covid-19 kufikia tisa.
Wagonjwa hao wapya wanane wote ni raia wa Uganda ambao wamerejea nchini humo kutokea Dubai baina ya tarehe 20 na 22 mwezi huu.
Waziri wa Afya wa Uganda, Jane Ruth Aceng amewaambia wanahabari kuwa kufikia sasa nchi hiyo imebaini wasafiri 2,661 wakiwemo raia wa nchi hiyo ambao wanaweza kuwa na hatari ya kusambaza maambukizi na watu wote hao wapo chini ya uangalizi maaalumu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...