Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya ametoa mwito kwa jamii ya kimataifa kushirikiana na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kipindi hiki cha kukabiliana na virusi vya Corona.
Josep Borrell ametoa mwito huo jana Jumatatu mjini Brussels na kuongeza kuwa, umoja huo unajiandaa kutuma misaada ya kibinadamu yenye thamani ya yuro milioni 20 hapa nchini Iran na Venezuela ndani ya wiki chache zijazo.
Kadhalika amesema EU inaunga mkono suala la Iran kupewa mkopo na Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) kutokana na hali ngumu inayopitia nchi hii iliyosababishwa na vikwazo vya Marekani.
Mapema mwezi huu, Benki Kuu ya Iran iliiandikia barua IMF, ikiomba mkopo wa dharura wa dola bilioni 5 kwa ajili ya kupambana na Corona, hii ikiwa ni mara ya kwanza kwa Jamhuri ya Kiislamu kuomba mkopo tokea ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya mwaka 1979.
Josep Borrell ametoa mwito huo jana Jumatatu mjini Brussels na kuongeza kuwa, umoja huo unajiandaa kutuma misaada ya kibinadamu yenye thamani ya yuro milioni 20 hapa nchini Iran na Venezuela ndani ya wiki chache zijazo.
Kadhalika amesema EU inaunga mkono suala la Iran kupewa mkopo na Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) kutokana na hali ngumu inayopitia nchi hii iliyosababishwa na vikwazo vya Marekani.
Mapema mwezi huu, Benki Kuu ya Iran iliiandikia barua IMF, ikiomba mkopo wa dharura wa dola bilioni 5 kwa ajili ya kupambana na Corona, hii ikiwa ni mara ya kwanza kwa Jamhuri ya Kiislamu kuomba mkopo tokea ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya mwaka 1979.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...