Na Amiri kilagalila,Njombe
Mkuu wa Gereza la Ndulamo wilayani Makete mkoani Njombe amewaomba wadau mbali mbali kujitokeza kusaidia ukamilishwaji wa ujenzi wa zahanati ya gereza hilo ili kuokoa maisha na kuimarisha usalama kwa wafungwa na mahabusu ndani ya gereza.
Gereza la wilaya ya Mkete (Ndulamo) lililopo wilayani Makete, ni moja kati ya magereza yanayopatikana ndani ya mkoa wa Njombe.Moja ya changamoto kubwa hapa inayoelezwa na Aloyce kayela mrakibu mwandamizi wa magereza wilaya ya Makete ni kukosekana kwa huduma za afya kwa mahabusu na wafungwa wanaotumikia adhabu zao ndani ya gereza hili hususani pale wanapougua ghafla nyakati za usiku.
“kwa hiyo baada ya kukaa na kamati yangu tukabuni na kujitolea ngvu zetu kujenga zahanati ya ndani ambapo wafungwa au mahabusu watakapopata maradhi ya ghafla basi watahudumiwa ndani ya gereza”alisema
Magereza ni pahala ambapo watu huifadhiwa pindi wanapokiuka na kwenda kinyume na sharia za nchi lengo likiwa ni kujifunza na kurekebisha tabia zao.
Kwa kutambua umuhimu wa kuendelea kuwajali na kuwathamini kama watu wa kawaida,chama cha maendeleo wilayani Makete MDA wamejitolea mifuko ya saruji 40, Bati 40 na misumari,tayari kwa kuendelea na ujenzi wa zahanati ya gereza la Ndulamo.
“kwa hiyo tunaamini walihapa nao wana nafasi kubwa ya kutumikia nafasi zao za gereza lakini siku moja tuje kuungana nao kuleta maendeleo kwenye wilaya yetu kwahiyo huku ni lazima waweze kupata hata huduma za afya waweze kutoka salama”alisema Mpandila
Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya makete Veronica Kessy ambae ni Mkuu wa wilaya hiyo amesema kunahaja ya wadau kuendelea kujitokeza katika kusaidia ujenzi wa zahanati hiyo huku akiwapongeza viongozi na wanachama wa MDA kwa kutambua umuhimu wa zahanati hiyo.
“tayari mmeleta mabato arobaini,mifuko ya simenti arobaini mmeleta misumari nichukue nafasi kuwapongeza wana M.D.A na ninapata faraja kwamba mpo kwa ajili ya Makete”alisema Veronika Kessy
Aloyce Kayera Mkuu wa Gereza la ndulamo wilaya ya makete amepokea baadhi ya vifaa vilivyotolewa na chama cha maendeleo makete MDA huku akiwapongeza kwa kuguswa na kutoa kile walichojaaliwa.
Vile vile chama cha maendeleo Makete wamekabidhi fedha kiasi cha shilingi milioni moja na laki mbili kwa ajili kuhakikisha umeme unafika katika nyumba za walimu wa shule ya sekondari ya wasichana Makete.
 Mkuu wa wilaya ya Makete Veronica Kessy pamoja na viongozi wa chama cha maendeleo Makete wakionesha moja ya msaada uliotolewa na wanachama wa chama cha maendeleo makete M.D.A
 Zahanati ya magereza Makete inayosaidiwa baadhi ya vifaa kwa ajili kukamilisha ujenzi
 Mkuu wa wilaya ya Makete Veronica Kessy wakati akizungumza kabla ya kupokea msaada.
  Katibu wa chama cha maendeleo Makete Award Mpandila akizungumza kabla ya kukabidhi msaada wa bati misumari na mifuko ya saruji

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...