Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

MCHEKESHAJI maarufu na mkongwe kutoka Japan Ken Shimura (70) amefariki dunia usiku wa kuamkia leo mjini Tokyo baada ya kupata maambukizi ya Corona baada ya kupata maambukizi ya virusi vya Corona (covid 19) Shirika la Utangazaji CNN na watu wake wa karibu wamethibitisha.

imeelezwa kuwa Shimura aliumwa homa ya mapafu kufariki dunia jumapili usiku, huku ikielezwa kuwa alianza kusikia dalili ikiwemo uchovu Machi 17 na alilazwa Machi 20 kabla ya kugundulika kuwa na virusi hivyo Machi 23 mwaka huu.

Shimura alianza shughuli ya uchekeshaji mwaka 1974 akiwa kivutio kwa wajapani wengi kupitia kundi la "Drifters".

Japan kupitia Wizara ta afya imetangaza visa 173 vya virusi vya Corona (covid 19) huku visa 68 vikitokea Tokyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...