NA TIGANYA VINCENT

MKUU wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wilaya ya Sikonge kumkamata Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Tutuo Longa Magasha na kuchunguza tuhuma za malipo ya fedha ya milioni moja kwa kazi hewa ya ukarabati wa kisima.

Alisema kiasi hicho cha fedha zilitolewa kupitia fedha ambazo Zahanati hiyo ilipata kutokana na Malipo kwa Ufanisi (RBF) kwa lengo kufanyia ukarabati wa kisima lakini haionyeshia kama kuna kazi imefanyika.

Mwanri ametoa kauli hiyo jana wakati wa ziara ya ukaguzi wa utekelezaji wa shughuli za Malipo kwa Ufanisi (RBF) kwenye Vituo na Zahanati mbali katika Wilaya ya Sikonge.

Alisema baada ya kumhoji Mhasibu wa Zahanati hiyo alimweleza kuwa Mganga huyo kupitia Dokezo alimtaka amlipe yeye kiasi cha fedha hizo ili akawalipe mafundi na vibarua walioshiriki kazi ambayo haionekani.

Mwanri alisema Mganga huyo asimame kupisha uchunguzi wa TAKUKURU kama itaonyesha kumefanyika wizi wa fedha za umma apelekwe Mahakamani na kama itaonyesha hakuna kosa basi aendelee na kazi yake.

Akizungumza katika mkutano huo Mkuu wa TAKUKURU wilayani Sikonge Magore Msena alisema walishapata taarifa za matumizi mabaya fedha za umma katika mradi huo wa kisima na walikuwa wakiendelea na uchunguzi na walikuwa mbio kuwachukulia hatua wahusika.

Alisema uchunguzi wa awali walibaini kuwa ni kiasi cha shilingi milioni mbili na sio milioni moja ndio kinaonekana kutumika katika kazi hiyo hewa .

Mkuu wa Mkoa wa Tabora akiwa wilayani Sikonge amefanikiwa kukagua Kituo cha Afya Mazinge, Zahanati ya Tutuo, Zahanati ya Pangale na Zahanati ya Usesula.
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akizungumza jana na wagonjwa katika Zahanati ya Tutuo wilayani Sikonge wakati wa ziara ya ukaguzi wa utekelezaji wa shughuli za Malipo kwa Ufanisi (RBF) kwenye Vituo na Zahanati mbali katika Wilayani humo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...