TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI.

KUINGIZA GARI NCHINI BILA KIBALI.

Jeshi la Polisi mkoani Mbeya linawashikilia watuhumiwa wawili BAKARI WALII SEMVUA [31] Mfanyabiashara na mkazi wa Mbagala Jijini Dar -es- Salaam na VICTOR JIMMY BROWN [25] Dereva/fundi, mkazi wa Tabata Segerea Jijini Dar -es- Salaam kwa tuhuma za kuingiza Gari nchini bila kibali.

Watuhumiwa walikamatwa mnamo tarehe 17.03.2020 majira ya saa 19:50 usiku huko eneo la Mafiati, Kata ya Manga, Tarafa ya Sisimba, Jiji la Mbeya katika barabara ya Mbeya – Iringa baada ya Jeshi la Polisi kuweka mtego na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wakiwa na Gari hilo lenye namba za usajili T.515 DNK aina ya BMW rangi ya blue na Chassis Namba.WBA 52030CK64536 kutoka nchini Zambia wakiwa wanaelekea Dar es Salaam.

Baada ya kuikamata gari na watuhumiwa walifanyiwa mahojiano kwa kuwashirikisha Maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tawi la Mbeya [TRA] upande wa ushuru na forodha na kubaini kuwa Gari hiyo iliingizwa nchini kama IT na kusafirishwa kupelekwa Tunduma kwa lengo la kupelekwa nchini Zambia ambapo ilifikishwa mpakani Tunduma tarehe 07/03/2020 ikiendeshwa na mtuhumiwa BAKARI WALII SEMVUA lakini ilipofika tarehe 17/03/2020 dereva huyo akiwa na VICTOR JIMMY BROWN waliamua kuondoka/kuiba Gari hiyo huku wakiwa wameweka “plate” namba T.515 DNK ambayo siyo ya Gari hilo. Upelelezi unaendelea.
 

KUKAMATWA KWA WATUHUMIWA WA KUVUNJA GHALA MCHANA NA KUIBA.

Jeshi la Polisi mkoani Mbeya linawashikilia watuhumiwa wawili [02] FREDY NGODOKI [34] Afisa Mauzo wa Kampuni ya “Chang Qing” inayojihusisha na utengenezaji, usambazaji na uuzaji wa Magodoro aina ya Ocean Kiss, Fahari na Okle na THADEI MATAMBA [30] Mfanyabiashara na Mkazi wa Veta Mbeya kwa tuhuma za kuiba na kuuza Magodoro 161.

Watuhumiwa walikamatwa katika msako mkali uliofanywa na Jeshi la Polisi mkoani hapa kuanzia tarehe 21.03.2020 na 22.03.2020 katika maeneo ya Jiji la Mbeya, Mbalizi na Itaka Kijiji cha Ikonya Wilaya ya Mbozi, Mkoa wa Songwe na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa ambapo FREDY NGODOKI amekiri kuiba magodoro yenye size tofauti 161 yenye thamani ya Tsh. 12, 500, 000/= na kisha kuyauza kwa THADEI MATAMBA.
Aidha baada ya mahojiano, mtuhumiwa THADEI MATAMBA amekiri kuuziwa magodoro 143 kwa thamani ya Tsh 10, 000,000/= na kupewa risiti lakini amekiri kuwa alikuwa bado hajalipa pesa.

Katika msako huo, jumla ya magodoro 89 yamepatikana nyumbani kwa mtuhumiwa THADEI MATAMBA. Katika ufuatiliaji mtuhumiwa FREDY NGODOKI amekiri kuuza magodoro mengine 10 huko maeneo ya Uyole. Upelelezi wa shauri hili unaendelea.

WITO:
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi ULRICH MATEI anatoa wito kwa wananchi kufuata sheria na taratibu zilizopo ili kujiepusha na matatizo/usumbufu pindi wanaponunua na kuagiza bidhaa mbalimbali kama vile magari. Aidha anaendelea kutoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu ili waweze kukamatwa na kuchukulia hatua stahiki kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za nchi.

Imetolewa na:
[ULRICH O. MATEI – SACP]
   KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...