Wana CAMA ni mtandao wa wasichana waliofadhiliwa na shirika la CAMFED kupata elimu. Katika kudhimisha siku ya Wanawake Duniani wana CAMA walijumuika na wanawake wengine katika wilaya za Kilosa, Gairo, Morogoro,  Ifakara, Kilombero, Kibaha, Chalinze, Rufiji, Kibiti, Kilolo, Handeni DC, Handeni TC, Iringa na Pangani,   kuadhimisha siku hiyo kwa kishindo. 
 Baadhi ya mabinti waliofadhiliwa na CAMFED (wana CAMA)  kusoma ufundi wa magari katika chuo cha wananchi Handeni (Folk Development Collage) wakionyesha uwezo wao katika madhimisho ya siku ya wanawake wilayani Handeni.

Mkuu wa wilaya ya Morogoro mjini Bi. Regina Chonjo akipokea msaada wa mabox ya taulo za kike uliotolewa na wafadhiliwa wa CAMFED (wana CAMA) wa wilaya ya Morogoro kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake wilayani Morogoro. Huu ni utaratibu waliojiwekea wana CAMA hawa kuhakikisha wanarudisha mafanikio yao kwenye jamii.


Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Bi. Asiah Abdallah aliyekua mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya mwanamke wilayani kilolo akitazama bidhaa za mafuta ya kupikia zinazozaliswa na wana CAMA wa wilaya ya kilolo.



 Baadhi ya wana CAMA kutoka wilaya mbalimbali hawakubaki nyuma katika kuonyesha umahili wakutengeneza bidhaa mbalimbali zikiwemo asali, unga wa ugali, na utengenezaji wa chaki.

 Wana CAMA walikua pia na ujumbe wakumlinda mtoto wa kike kuhakikisha anafikia ndoto zake.
Baadhi ya wasichana waliofadhiliwa na CAMFED  (wana CAMA)  kusoma ufundi wa umeme katika chuo cha wananchi Handeni (Folk Development Collage) wakionyesha uwezo wao katika madhimisho ya siku ya wanawake wilayani Handeni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...