Ghasia zimeshuhudiwa katika viwanja vya ndege vya Marekani wakati ambapo hatua mpya za ukaguzi kwa sababu ya virusi cha Corona zinaanza kutekelezwa dhidi ya watu wanaorejea nchini humo kutoka Ulaya.

Kumekuwa na foleni ndefu huku wasafiri wakisubiri kwa saa kadhaa kukaguliwa kabla ya kupita kwenye ofisi za forodha.

Awali, Makamu Rais wa Marekani Mike Pence amesema kuwa Uingereza na Ireland Jumanne zitaongezwa kwenye orodha ya nchi zilizopigwa marufuku kuingia nchini humo pamoja nchi zingine za Ulaya zilizotambuliwa.

Marekani ina visa zaidi ya 2,700 vya corona huku vifo 54 vikiwa tayari vimethibitishwa.

Wachambuzi wanasema kwamba, kwa sasa hali ya taharuki imetanda nchini Marekani huku kukiwa na hofu ya huduma za hospitali kutoweza kufikia wote wenye hitaji la haraka pamoja na huduma kwa watoto wakati ambapo mamilioni ya wanafunzi wanarejea nyumbani.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...